Monday, October 27, 2008

SIO KUSUKA MIKEKA TU HATA KUKAA SIKU NZIMA KUSUBIRI WATEJA NI MOJA YA KUJITEGEMEA

Sijui kama wenzangu mnaona sawasawa wanauza nini. Ah ngoja niwaambia ni kwenye ndoo ni bamia lita mia nna, kwenye ungo ni uyoga bakuli mia tatu, kwenye ungo mwingine kumbikumbi kikombe mia mbili na halafu karoti fungu mia moja.

2 comments:

Unknown said...

Umenikumbusha mbali sana! Nimewahi kubeba mzigo wa maharage ukijitwisha hakuna kutua hadi ufike km 20, ukitua hakuna wa kukutwisha. Ukifika sokoni uombe Mungu upate mteja kwani ukikosa itabidi urudi kwenu bila pesa ambayo ni ada ya shule.
Lazarus

Yasinta Ngonyani said...

mmh maisha kweli ni safari ndefu. kujitegemea kujitegemea, watu tumetoka mbali sanaaaaaa mungu tu anajua