Tuesday, October 14, 2008

KUMBUKUMBU YA MANENO ALIYOSEMA HAYATI BABA WA TAIFA JULIUS K. NYERERE

"Uongozi unaweza ukwa mzuriau mbaya, au usijali, lakini kama watu wameamka na wanajitambua wenyewe, kutoshirikishwa kwa mawaza na tabia ya jamii hakutaendelea kwa muda mrefu".

NYERERE:- BORA NINGEKUWA MHUBIRI WA DINI KULIKO KUWA RAIS WA NCHI!

Baadhi ya maneno ya hayati Mwalimu, alipofikisha umri wa miaka 50"..Wakati nikiwa Makerere, niligundua kwamba serikali ya nchi yangu ilikuwa ikinilipia kiasi cha paundi 80 kila mwaka kwa ajili ya elimu yangu. Lakini hio haikuwa na maana kubwa sana kwangu, isitoshe paundi 80 ni chembe ndogo tu ya kiasi cha jumnla ya pesa zinazokusanywa na kutoka kwa walipa kodi wa nchi yangu, yaani wa-Afrika. Leo hii, paundi 80 ziimeongezeka thamani yake na kuwa na maana kubwa kwangu. Siyo kwamba ni zawadi muhimu tu na tunu kwangu, lakini pia ni deni ambalo kamwe sitaweza kulilipa.""Sina uhakika kama wengi wetu wamepata kufikiria kwamba wakati paundi 80 zilikuwa zinatyumika kunitunza mimi kule Makerere, hela hizo zingeweza kujenga Zahanati angalau mbili katika kijiji changu au chochote kingine Tanzania."".. Inawezekana kabisa kuwa wananchi walikuwa wanakufa kwa ukosefu wa dawa kwa sababu tu ya kukosa paundi zile 80 zilizokuwa zikilipwa kwa ajili yangu. Kwa hiyo kuwapo kwangu chuoni kuliinyima jamii huduma ya wale wote ambao wangeweza kusomeshwa kwenye shule chini ya miti, na kuwaandaa kina Aggreys na Booker Washingtons, Je nitawezaje kamwe kutolilipa hilo deni kwa jamii yangu hii?.""Jamii inatumia fedha zote hizo kwa ajili yetu kwa sababu inataka tuwe nyenzo za kuiinua jamii hiyo. Kwa hiyo lazima siku zote tubakie chini ya jamii hiyo na kuhimili uzito wote wa wananchi ambao wanahitaji kuinuliwa, na lazima tusaidie kuifanya hiyo kazi ya kuwainua wananchi wasiojiweza"Wakati nikisoma matukio yaliyojiri kuelekea kifo cha Babu (Sokoro) kama tulivyozoea kumuita, machozi yamenidondoka sio tu kwa sababu ya kuondokewa na mtu muhimu kwangu na Taifa, bali pia kwa kukosa nafasi ya kutimiza nadhiri yangu ya kumpa shukrani japo ya ahsante kwa mema aliyonitendea mimi pamoja na mafanikio aliyonitabiria tarehe 2.1.1987. Pia nalia kwa sababu baada ya kuonana naye wakati alipotembelea maonesho ya Sabasaba mwaka 1999, sikumuona tena zaidi ya alipokuwa ndani ya jeneza pale Msasani na Butiama.Lakini nalia zaidi ninapokumbuka kuwa baada ya kifo chake, watu wengi wamikuwa victimized kwa sababu ya misimamo ya kiuadilifu. Wazalendo wamekuwa wakitemewa mate na kupewa majina ya huyo siyo MWENZETU (katika ufisadi) n.k. Waovu katika jamii wamepewa majina ya Huyo mjanja n.k. Nitaendelea......... machozi yamelowanisha Key Board mpaka imestark.

No comments: