Wednesday, October 22, 2008

MALARIA NI UGONJWA HATARI

Habari za ziku mbili hizi nilikuwa katika harakati za kuitafuta picha hii. Ngoja tuiangalie kidogo nadhani wote mmegundua ni nini. Hata hivvyo nitawaeleza kidogo.




Hapa ni mnaona jinsi malaria yanavyoharibu chembechembe za damu(blood cell) katika miili yetu. Malaria aina hii yanaitwa malaria malaria. Ilikuwa mwaka 2001 wakati tulipokuwa Tanzania, nilitaka kumpoteza mume wangu kwa homa hii ya malaria. Nina maana vidudu hivi vya malaria mnavyoviona vilikuwa mwilini mwake.

2 comments:

Christian Bwaya said...

Kwa namna miili yetu inajua kupambana na ugonjwa huu, binafsi naona huu ni ushahidi kwamba mwafrika ni ngangari kuliko aina yoyote ile ya binadamu katika sayari hii. Sisi tunaugua malaria na tunapona juu kwa juu bila hata kidonge. Mbu wanakula mapaka asubuhi, hakuna maleria.

Wale jamaa zetu, malaria maana yake ni tiketi ya kuzimu. Kuna haja ya kufanya utafiti wa kinga mwili tulizonazo waafrika. Kwa nini zinawazidi wale wenzetu?

Tujipende watu weusi. Tumependelewa.

Yasinta Ngonyani said...

Asante kwa maoni bwaya, lakini nina swali moja je? kuna watoto wangapi kila wanakufa kwa malaria Tanzania?