Friday, October 24, 2008

KWA AJILI YA WIVU AMEPELEKA CHUPI YA MKEWE IPIMWE DNA

Hiki ni kisa cha Antoni na Ana. Baada ya miaka 18 ya ndoa, Ana hataki tena kufanya tendo la ndoa na Antoni. Na Antoni ameshuhudia kwa macho yake mkewe Ana akipigwa busu na mfanyakazi mwenzake wakati wakiwa wanasubiri basi kwenda kazini. Halafu amekuta picha ya yule mwanamume aliyembusu mkewe kwenye pochi ya Ana.

Kwa hiyo hapo inaonyesha ya kwamba Ana anatoka nje. Na Antoni hayaamini maelezo ya Ana kwa nini hataki kufanya tendo la ndoa naye wala kubuswa. Antoni anasema katika maisha yake hakuweza kuwaza ya kwamba mkewe Ana angeweza kumtendea hivyo. Hakujua kama hangeweza kumwamini mke wake,

Majibu ya DNA yamerudi ni kweli kulikuwa na shahawa kwenye chupi, lakini asilimia 100% zinaonyesha kuwa ni shahawa zake yeye Antoni. Baada ya hapo aliamua kuacha kila kitu na pia kutokuwa na haraka za kupeleka vyupi vya mkewe kwani inaonyesha ulikuwa wivu tu. Kwa hiyo tangu siku ile Antoni na mkwe Ana walikuwa na furaha na amani tena katika ndoa yao.

Ana pia alielewa kwa nini mume wake Antoni aliangaika kupima chupi na kumfikiria vibaya. Antoni anasema sasa anamwamini mkewe katika maelezo kuhusu hisia ambazo alikuwa nazo kwa mfanyakazi mwanzake ya kuwa ilikuwa sio mapenzi.

Antoni anasema, Wakati wa kufanya tendo la ndoa alikuwa na makosa kwani aliamini mke wake anatoka nje. sasa mapenzi yao huwezi kufananisha na miaka yote iliyopita, anasema Anton.
SWALI:- Je? ungekuwa wewe ndio ungefanya kama alivyofanya Antoni?
Na J? ungekuwa wewe ndio Ana ungefanyaje?

No comments: