Friday, October 3, 2008

MAISHA YA KAZI

Ungekuwa wewe unafanya kazi halafu unaona mfanyakazi mwenzako anafanya mambo si mazuri. Yaani kinyume na sheria. Je ungemwita na kumwambia au ungemwacha tu aendelee. Kwa sababu naona kuna watu wengi wanasema/wanatetena fulani yule mmh anatabia mbaya sana au angalia kwanza anategea kweli, hafanyi kitu. Hasa sisi akina dada/mama. Kwa nini usimwite na kumwambia/ongea naye, pengine yeye anaona anafnaya kazi nzuri kabisa. Je wote tupo hivyo

1 comment:

Fita Lutonja said...

hakika kama mimi dada yasinta nitamuita na kumueleza kuhusiana na tabia yake hiyo na nitajitahidi sana kumufanya anielewe ili aache tabia hiyo