Friday, May 3, 2013

HUU NI MLO WANGU WA JANA JIONI ..KAZI YA MIKONO YANGU!!!

Hapa chakula ndo kinatoka tu kwenye oven...ni lasagne,,nyama ya kusaga, aina ya pasta, chizi na maziwa..dakika 30 kwenye oven.
 
 
Na hapa ni sahani ya Kapulya ..bila kusahau saladi na kinywaji ni maji

10 comments:

Said Kamotta said...

Huh, chakula hicho kinaonekana kuwa ni kitamu....kazi ni kula tu hapo.

Yasinta Ngonyani said...

Kaka Said.......Ahsante. .. kweli kitamu sana karibu..

Anonymous said...

Dada Yasinta jamani mie ni mgeni wako tangu muda ulipopika hicho chakula ukatuwekea hapa, nimekikumbuka! Jamani mie mgeni wako wa ghafla siku moja utaniona hapo kwako. Manake hicho chakula usifaidi mwenyewe sie wengine tunalia macho na hamu, au unipostie nini? Sijui nikupe anwani yangu hapa kwa kuwa nipo Sweden nadhani kitafika siku hiyo hiyo unaweka express ya stempu, kwa kweli hongera kwa mapishi mazuri.

Anonymous said...

Nimekumbuka tena hakitachacha, then chombo chako nitakupostia kukirudisha. Nipo serious anwani utaipata muda sio mrefu ngoja niitafute aah!

Ndugu Nkwazi N Mhango said...

Wow! Yummy pizza!

Yasinta Ngonyani said...

Usiue na jina .....hamna taabu hata chombo kaaanacho
Tu..otakuwa raha kulufahamu wewe ni nani su utanipa anuwani isiyo na jina ? Ahsante kwa kupenda mapisho yangu.

Mwal. Mhango Karibu. ..no kweli yummy wai sasa:-)

Anonymous said...

Umenichekesha kuwa ntakupa anwani isiyo na jina!Utanifahamu muda sio mrefu ´kwani bado natafuta anwani sijui nimeiweka wapi aah! baadae kidogo.

Mija Shija Sayi said...

Restaurant lini?

Yasinta Ngonyani said...

Usiye na jina utaitafutaje anwani ...maaana ni kitu muhimu saana huwezi kusahau...nimesema hivyo kwa vile huna jina ...

Dada mkuu msaidizi. ..duh! Huko tena...ahsante kwa wazo:-)

ray njau said...

Huyu ndiye mtoto wa kike(Yasinta binti Dadi Ngongani kutoka Ruhuwiko Mkoa wa Ruvuma nchini Tanzania) na stadi zake za mapish.Huu ni udhibitisho dhahiri wa mwanamke mwenye kusimamia madaraka na nafasi yake katika familia.Kamwe uvivu siyo stadi rafiki katika mchakato wake(Yasinta binti Dadi Ngonyani) wa maisha na mafanikio kuanzia machweo hadi mawio.Usengwili mau!!