Sunday, May 26, 2013

NA HAPA NI BAADHI YA ZAWADI NILIPONGEZWA KWA SIKU HII YA AKINA MAMA/MORS DAG!!

 Kutoka kushoto ni kikombo cha chai ambacho kina chunjio na mfuniko wake si mnajua nilivyo mpenzi wa chai, hicho cha maji ya bahari ni flip cover kwa ajili ya simu yangu, ya tatu ni sceen protertor, nilipata na bahati nasibu /TRISS, ila bahati mbaya sijapata bahati nasibu.. NA MWISHO hicho mkionacho cha bluu ni kwa ajili ya kuhifadhi simu yangu nikimbiapo maana huwa napenda kusikiliza miziki......haikuishia hapo nikaandalia...
....keki na ni dada Camilla ndiyo aliyetengeneza keki hii maalumu kwa ajili ya mama---inaitwa rabarberkaka/keki ya rhubarb...karibuni bado ipo......

13 comments:

Ndugu Nkwazi N Mhango said...

Yummy, yummy cake! Nakutakia sherehe njema na bab kubwa. Mbarikiweni jamani. Faidini majira haya ya joto baada ya kukong'otwa na baridi ya winter.

Yasinta Ngonyani said...

Mwal. Mhango ! Ahsante ...ni kweli baridi ilikuwa kali na bado ipo ..lakini leo nimekuwa nje na ndala , sketi na t-shirt tu :-D

Anonymous said...

Hongera sana Yasinta.
Keki tumekula kwa macho, mwambie Camilla ilikuwa tamu sana! Siku ingine apike special kwa ajili wa wanablog wa mama tu. haya mie wa kupostiwa sijui keki ntaipata?

Mija Shija Sayi said...

Hongera kwa zawadi, unastahili kwa kweli...Hivi Camilla kumbe ni mpishi mzuri hivi?

Mpe hongera zangu..

ray njau said...

Hongereni sana!!

Unknown said...

duh! hongera sana dada. Sasa hiyo keki ndio tinekula pekee bila kutualika?

Yasinta Ngonyani said...

Udiye na jina wala usikonde atatengebeza tu maana anapenda mno kuoka....

Dada mkuu msaidizi! Ahsante. ..jana nilistarehe kweli. Mija mtoto wa nyoka ni nyoka.

Kaka Ray. ..ahsante.

Kaka mrope..kwanza karibu tena nimekumiss. ..ahsante kaka. Kaka si nimesema hapo juu karibuni..karibu alo

Unknown said...

Mwe wajameni tutakaribia sana tu. hakikisha ni vya kutosha kwa wote

Yasinta Ngonyani said...

Kaka Mrope! Wala usikonde utaacha mwenyewe, wewe njoo tumbo waziiiii

Anonymous said...

mh namashaka na hizo budget zenu nje!kuna kushiba kweli au maneno tu.

Yasinta Ngonyani said...

Usiye na jina! Ukija utajionea mwenyewe. Hakuna gaja ya kuandikia mate.....

Rachel Siwa said...

Duuhh nilipitwa "KACHIKI" Hongera sana KADALA na kina MAMA wote, Bila shaka keki nimewekewa..kizuri kula na nduguyo!!!!!

Yasinta Ngonyani said...

Kchiki! Si unajua hakuna kuchelewa...Ahsante na hongera nawe pia kuhusu keki usikonde:-)