Saturday, June 2, 2012

UJUMBE WA JUMAMOSI YA LEO..MAISHA!!!


Katika maisha inabidi tuwe makini. Maisha yapo kama yalivyo. 
Na kama haturidhiki nayo :- Basi tuchukua uamuzi na kuyabadili.
JUMAMOSI NJEMA NDUGU ZANGUNI

5 comments:

ray njau said...

Je, Hivi Ndivyo Mungu Alivyokusudia?
==================================
KATIKA magazeti, televisheni, na redio, kuna habari nyingi kuhusu visa vya ugaidi, vita, na uhalifu. Hebu fikiria pia mahangaiko yako mwenyewe. Labda unasumbuliwa na ugonjwa fulani au umefiwa na mtu unayempenda. Huenda ukahisi kama alivyohisi Ayubu, aliyesema kwamba maisha yake yalikuwa ‘yamejaa masumbuko.’—Ayubu 10:15, Verbum Bible.

Hebu jiulize:

Je, hivi ndivyo Mungu alivyokusudia maisha yangu na ya wanadamu wengine yawe?
Ninaweza kupata wapi msaada wa kukabiliana na matatizo yangu?
Je, dunia itapata kuwa na amani?

Biblia inajibu maswali hayo kwa njia ya kuridhisha.
----------------------------------
BIBLIA INAFUNDISHA KWAMBA MUNGU ATATIMIZA MAMBO HAYA DUNIANI.
-----------------------------------
Mtu aliyekuwa mzee awa kijana tena

“Atafuta kila chozi kutoka katika macho yao, na kifo hakitakuwapo tena, wala maombolezo wala kilio wala maumivu hayatakuwapo tena.”—Ufunuo 21:4

Msichana aliyekuwa mlemavu aanza kukimbia tena

“Kilema atapanda juu kama vile paa anavyofanya.”—Isaya 35:6

Mtu aliyekuwa kipofu aanza kuona tena

“Macho ya vipofu yatafunguliwa.”—Isaya 35:5

Mwanamke akifurahia kumwona mpendwa wake aliyefufuliwa

‘Wale wote waliomo ndani ya makaburi ya ukumbusho watatoka.’ —Yohana 5:28, 29

Mvulana aliyekuwa mgonjwa apona

“Hakuna mkaaji atakayesema: ‘Mimi ni mgonjwa.’”—Isaya 33:24

Mashamba ya nafaka

“Kutakuwa na wingi wa nafaka duniani.”—Zaburi 72:16

FAIDIKA NA MAFUNDISHO YA BIBLIA
Wanaume wawili wakijifunza Biblia

Usidhani kwamba mambo hayo ni ndoto tu. Mungu ameahidi kwamba atatimiza mambo hayo, na Biblia inaeleza jinsi atakavyofanya hivyo.

Hata hivyo, Biblia ina faida nyingine nyingi. Inaweza kukusaidia kuwa na maisha yenye kuridhisha hata sasa. Hebu tua kidogo, ufikirie mahangaiko na matatizo yako mwenyewe. Huenda yanatia ndani ukosefu wa pesa, matatizo ya familia, matatizo ya afya, au kifo cha mpendwa. Biblia inaweza kukusaidia kushughulika na matatizo leo na inaweza kukufariji kwa kujibu maswali kama haya:

Kwa nini tunateseka?
Tunawezaje kushughulika na mahangaiko ya maisha?
Tunawezaje kufanya maisha ya familia yetu yawe yenye furaha zaidi?
Inakuwaje tunapokufa?
Je, tutapata kuwaona wapendwa wetu waliokufa?
Tunawezaje kuwa na hakika kwamba Mungu atatimiza ahadi zake kuhusu wakati ujao?

Kusoma kitabu hiki kunaonyesha kwamba ungependa kujua yale ambayo Biblia inafundisha. Kitabu hiki kitakusaidia. Sehemu ya chini ya kurasa kuna maswali yanayoambatana na mafungu. Mamilioni ya watu wamefurahia kuwa na mazungumzo ya Biblia pamoja na Mashahidi wa Yehova kwa njia ya maswali na majibu. Tunatumaini kwamba wewe pia utafurahia kufanya hivyo. Mungu na akubariki unapochukua hatua hiyo yenye kusisimua na kuridhisha ya kujifunza mambo ambayo Biblia inafundisha hasa!
IJUE BIBLIA YAKO
Biblia

KUNA vitabu 66 katika Biblia. Kila kitabu kina sura na mistari, ili kurahisisha usomaji. Maandiko yanapotajwa katika kitabu hiki, nambari inayofuata jina ndiyo sura ya kitabu au barua katika Biblia, nayo nambari inayofuata ni mstari. Kwa mfano, “2 Timotheo 3:16” ni barua ya pili kwa Timotheo, sura ya 3, mstari wa 16.

Mbona usianze kuisoma Biblia kila siku? Ukisoma sura tatu hadi tano hivi kila siku, unaweza kuisoma Biblia nzima kwa mwaka mmoja.

Rachel Siwa said...

Asante kwa Ujumbe da'Kadala, j'Mosi iwenjema kwenu pia hapo nyumbani woote!!!
Mwali upendeza!!!!!

Wenu Kachiki.

o'Wambura Ng'wanambiti! said...

Aksante kwa ujumbe...

Na Umetokezeaaaaaaaa!

Interestedtips said...

mimi hicho kitenge kimenikumbusha mbaliiiiiiiiii, aaahh Bujumburaaa

MARKUS MPANGALA said...

kyani dada, mawazo?