Tuesday, June 12, 2012

JAMANI MNAKUMBUKA HADITHI HII BAADHI YETU TULISOMA TULIPOKUWA DARASA LA TATU :- JOGOO ALIYESEMA




Kumbukumbu ni nzuri jamani leo nawasomea wanangu nao wananisomea ...nimeona niwakumbushe na wenzangu pia si vizuri kuwa mchoyo.

6 comments:

Interestedtips said...

Pazi alikuwa mtoto mbaya.......vitabu vya zamani vilikuwa na hadithi za kufikirika

emuthree said...

Ndio vipo hivyo, kama akina Bulicheka, sungura na fisi,na kuna vitabu kama vile vya elifu lela ulela,Abunuasi...n VINGINEVYO,.duuh,nilipenda SANA kuvisoma.
Ndugu wangu,nilichogundua karne hizi, watoto wetu hawapendi sana kusoma, wanapenda sana kuangalia....komputa zinalemezaakili ya kusoma,..hesabu......

ray njau said...

Hakika ya kale ni dhahabu!!

D. Mkanula said...

da Yasinta hivi una kitabu cha Maisha Na Mafanikio? Sina uhakika kama mwandishi ni Munga Tehenan ila nimewahi kukisoma na kikanisaidia kuondokana na msongo wa mawazo. Kwa bahati mbaya nikakipoteza, kuna ndugu yangu ana matatizo na ningependa akisome kitabu hiki. Naishi Dar nimejaribu kukitafuta nimechemka, hata hapa kijijini kwako niibukia tu nikiwa ktk harakati za kukitafuta mtandaoni. Nisaidie kwa namna yoyote kama unaweza kukipata.

Salehe Msanda said...

Hadithi na stori za zamani zilikuwa na mafundisho yenye mshiko.



Nadhani bado unakumbuka vitabu vya kusoma vya juma na roza,damasi na lucy. bulicheka na mke wake lizabet na mpiga filimbi wa merini.
Vilikuwa vinaleta raha.
Na umenikumbusha kisa cha mwanafunzi mwenzetu aliyekuwa amekariri kusoma huyu ni Juma,juma na dada yake juma niroza. Lakini alikuwa akiambiwa aonyeshe hilo neno juma na roza ilikuwa kesi.
Hizo sawa na kukumbusha nyimbo ya msondo inayosema tulikotoka ni mbali sana.........
Inasadikiwa kuwa historia huwa inajirudia haya yanaweza kujirudia au.

Anonymous said...

Umenikumbusha mbali sana sana, tupostie na hadithi nyinyi kama vile shairi la karudi baba mmoja