Tuesday, April 17, 2012

NDIZI:- NI KATI YA VYAKULA NILIVYOKUWA NA UDHAIFU/NIVIPENDAVYO!!!

Mmmmhhh! sijui ni mara ngapi nimekodolea macho mlo huu wa ndizi leo. Ningependa kweli kula jioni hii hizi ndizi Bukoba..ila basi nakula kwa macho tu...Picha kutoka kwa Da´Lady Jay Dee .

9 comments:

ray njau said...

Asanteni sana kwa ndizi.

Yasinta Ngonyani said...

KakaRay! mwenzio hapa nipo hoi mate yanachirizika sio kawaida:-(

kokusimah said...

We da Yasinta unaendelea kuua nduguyo hapa, ndizi ugonjwa wangu na mate yananchuruzika hapa mpaka mwisho wa mwezi mhindi azilete nshakoma. Nimeipenda blog yako. Pamoja tuendeleze libeneke.

ray njau said...

Kizuri kula na nduguzo na kichungu meza mwenyewe.

Mija Shija Sayi said...

Sijui mkono wa nani huu..

batamwa said...

"egyo tugyetya kokoyangemu" yasinta mwambie kamala akutafasirie

EDINA-MIKAELA JOHNSEN said...

Yaani natamani hizi ndizi zigeuke ziwe za kweli..namiss nyumbani nikiona mambo kama haya.

Yasinta Ngonyani said...

Nachukua fursa hii, nami niseme machache tena chakula cha asili kwa kweli ni kitamu. Nawasikitikia wale wasiopenda kwa mfano ugali wa muhogo na mlenda pori...Ahsante wote kwa kuwa pamoja nami na kutamani chakula hiki kitamu..kula kwa macho...ruksa kuendelea kusema....

kamala Lutatinisibwa Lutabasibwa said...

mpunu yengemu egi. nyorobya kandi nyashamya mukulu @batamwa