Monday, September 7, 2009

KUSAIDIA KAZI ZA NYUMBANI + RUHUWIKO -SONGEA 2009

Namsaidia mama kuchambua maharage hapa ilikuwa mwaka huu 2009. Ruhuwiko.
Na mimi namsaidia mama kufua nguo hapa ilikuwa mwaka huu 2009. Ruhuwiko.





8 comments:

Mzee wa Changamoto said...

Hahahahaaaaaaaaaaa. Kina "Uncle" wanaendeleza kazi za ndani????
Hili la kazi pamoja na lugha ni mambo ninayojivunia saana kutoka kwako Da Y
Ukweli ni kuwa ni muhimu kwa watoto kujua umuhimu wa kazi za ndani. Hii huwafanya wathamini juhudi za wazazi na walezi wao wanapohangaika kuweka mlo mezani. Wasipojua "msoto" wake hawawezi kufikiri kuwa unatumia akili na busara kuwafanya waende mezani ama kuwalinda na maradhi ama kuwaweka safi ama kuwafanya wawe na mazingira yawe yalivyo
Nasi twaja nyuma yako. Si unajua eeeee??? Shhhhhhh. Usiseme
Blessings

Faith S Hilary said...

aaaaaaaaaaaw they are so cute!!!! Na ni vizuri wakijua kufanya vitu hivyo...but again, they are so cute!!!!

Mzee wa Changamoto said...

Candy unaweza hata kuchambua maharagwe wewe??? Kujipikilisha je? Namaanisha kupika sio Popcorn na Burgers za kuweka kwenye microwave. Lol
Just having fun ma LilHero

Fadhy Mtanga said...

Kinachonipa raha siyo kazi aifanyayo Camilla ya kuchambua maharagwe, angeweza kupretend ili afotolewe. Kinachonipa raha ni kwamba kazi yenyewe anaijua, halafu anaipenda.
Sema tu nd'o vile nilipofika kwa Mumyhery ndo mwisho wa reli. (tafadhali wajameni sijasema kitu kibaya msinichonganishe na mamkwe wangu)
Na Erik pia anaifurahia kazi yake.
Hongera sana da Yasinta. Unastahili sana sifa.
Upo juu.

chib said...

:-)

mumyhery said...

kuwakunja wakiwa wangali wabichi ni muhimu

Bennet said...

Hii safi sana, unafikiri akirudi huko atahadithia nini, ungempeleka na kuchunga mbuzi au ndama

Yasinta Ngonyani said...

Mzee wa Changamoto naamini kabisa hata wewe wakati utakapofika kuwa baba mwanao/wanao watajua hata kiHaya au nimekosea we si muHaya. Na pia nasema asante kwa kuona unajivunia kuwa nawafunza wanangu hayo.

Candy1! asante kwa yote najitahidi si unajua tamaduni mbili si mchezo.

Fadhy mtani! nafurahi kama umefurahi hilo na naamini nawe utakuwa baba mwenye kufunza wanao yale yote uliyofunza ulipokuwa mdogo.

Kaka Chib:-)

Mumyhery! Nashukuru kama unakubaliana nami.

Kaka Bennet Tayari wameshawahi kuchunga mbuzi na walipenda.