Thursday, December 18, 2008

JE? BINADAMU NA NYANI NI JAMII MOJA?

.............................Mrs. Ngonyani................Mr. Nyani

Aina hii ya nyani ipo zaidi katika nchi ya Gaboni tu. Angalia jinsi alivyo ni maalumu kidogo.Wanaitwa Mandrill.

6 comments:

Fadhy Mtanga said...

Hivi ni kweli?
Tatizo kumbukumbu yangu ina mgogoro. Nilipofundishwa somo la Historia, nilijifunza kuwa binadamu ametokana na nyani.
Nilipohudhuria Sunday School, nikafundishwa binadamu aliumbwa kwa mfano wa Mungu.
Mtu akinitegulia kitendawili hiki atakuwa amenisaidia.
Mtani eh, masikhara hayo, unataka kusema kina Mbawala, Komba, Mapunda, Matembo, Nguruwe, Mbogo, Nyati na kadhalika zote, nao wametokana na wanyama hao wenye majina yao?
Wajameni naomba nimbane mtani hapa hapa kwenye kumi na nane. Eti mtani, ushafanya kijiutafiti kuhusiana na haya majina yanayofanana na....
Kazi nzuri sana.
Bravo!

Anonymous said...

Naomba kuuliza swali dada Nangonyani. Swali langu ni matumizi ya Mr na Mrs. hivi mwanamke anapoitwa Mrs fulani, kwa mfano Mrs. Ngonyani, je, ina maanisha yeye ameolewa na bwana Ngonyani, au ni jina la ukoo wake (mwanamke?). Mimi binafsi nimekuwa nikielewa kwamba mwanamke anapoitwa Mrs fulani, manake kaolewa na mwanaume ambaye jina lake la ukoo ndio hilo fulani, kwa mfano wetu hapo juu, ninaelewa kwamba wewe Yasinta umeolewa na bwana Ngonyani. naomba kuwakilisha swali langu, nitashukuru kama nitapata ufafanuzi kwa wanajamii, maana hapa naona ni mahali pazuri pa kujifunza maisha na kadhalika.

ni mimi Ngalilihina (asiye na jina aka noname)

Unknown said...

Swali hili labda tumuulize BWAYA,
Yeye anweza kutusaidia zaidi.
Kuhusu swali la Mr. & Mrs. lililoulizwa na ASIYEJULIKANA, na mimi nasubiri jibu

Mzee wa Changamoto said...

Kuwa jamii moja sidhani kama yamaanisha moja kwa moja kuwa katokana naye. Nadhani twaweza kuwa jamii moja kisayansi kwa kushabihiana katika mambo mengi na nadhani ndio maana hata wanasayansi wanawatumia saana nyani katika kujaribu madawa ya binadamu kwa sababu kuna kufanana na ki-ujamii tuko karibu. Naweza sema tuko "karibu" kimaumbile jambo linaloweza kuchukuliwa kama jamii moja, lakini sina hakika kama nyani aligeuka kuwa mtu. Historia inakwenda mbaaali katika hili ila haisemi nyani alitoka wapi na wala chanzo cha nyani ni nini. Inanipa shaka kuamini hili. Ni namna nionavyo hili

Simon Kitururu said...

Topiki kubwa hii ingawa imejifisha katika mistari michache .

Cha uhakika ni wote tukifa tunageuka udongo.Kwa hiyo kwa waaminio Creation stories , labda wote tuliumbwa kwa udongo.

Hii topiki ukimuuliza aaminiye DARUWINI mtabishana mpaka juzi yake kuhusu jinsi gani viumbe vyote vina asili moja.

Hivi tulishapata jibu la kati ya kuku na yai nini kilitangulia ?

MARKUS MPANGALA said...

kuku na yai? hadithi murua, labda nyani na udongo? heee hapo patamu lakini kwani aliyeumbwa kwa mfano wa wake yaani mungu kwanini awe udongo? na pengine tuliumbwa toka sili moja kwanini tumbili wamebaki kama walivyo hee kumbe kuna kutoka nyani hadi binadamu? ndiyo kumbe yale ya MAN APES OR APES MAN? sijui au AUTHEPECAS{rekebisha herufi tafadhali} au yale ya ZINJANTHROPUS hee kumbe mungu alimumwa nyani? sijui na siisimiza ana umuhimu gani, pengine kuamini kuhusu DARWINI ni nafuu pia kuamini uumbaji ni afadhali .... lakini kwanini tunachokonoa hayo? si walisema watakuja wapingaji eti watapinga kristo heee? tusiulize basi tunyamaze kwanini tunafukiwa? au tukitupwa tunakuwa mizogo na kuoza kuwa udongo, ikawaje yale ya kutokea dunia ya akina Afred Wegener na Francis Bacon kwamba dunia ilikuwa LANDMASS tu ya PANGAE? halafu ukazaliwa Panthalasa na Laurasia? kisha.... yakatoea mabara tuliyonayo mmmmmm ushahidi eti matukio ya volkano, si mliona kule CHINA miezi ya karibuni milima ikawa maziwa makubwa, kwanini? pengine mungu aliumba... lakini yeye aliumbwa na nani? mbona anasema tuumbe mtu kwa mfano wetu, heee wengine walikuwa akina nani? labda shetani? labda tuache tu ...lakini mpka lini? kaka Simon unayo majibu tupatie na huyo Kalama, mzee wa changamoto, kaluse,bwaya. semeni basi mbona unamkuna videvu vinawasha au?
ha ha ha nimeshindwa sina jibu Yasinta mchokozi kama siyo mchokonozi mmm hii topiki kali sana lakini imo mokononi mwetu