Monday, March 4, 2013

JUMATATU YA LEO TUIANZE KWA KUANGALIA VIPI JUMAPILI YA JANA ILIKUWA KWA KAPULYA...MLO WA JUMAPILI JIONI ULIKUWA KAMA IFUATAVYO:- WALI, SAMAKI AINA YA COD NA SLAMON, MCHUZI WA NAZI NA NJEGERE!!!

 Hapa mishikaki ipo tayariinasubiri kuchomwa ni mishikaki ya samaki ya aina mbili:- cod na salmon anayejua kwa kiswahili anisaidie tafadhali nimetafuta sijapata jibu.
 ---na hapa tayari mishkaki imeiva ..nimechoma kwenye oveni kwa vile huko nje bado kuna baridi na theruji nyingi sana ....
Na hapa mlo mzima ndivyo ulivyokuwa wali, njegere, salmon,cod na mchuzi ulioungwa kwa nazi  jioni ya jana ilikwisha safiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii sana...
 
Na baada ya kula chakula kilibaki basi Kapulya akapata kutengeneza la kwa ajili ya kula leo jumatatu awapo kazini.Huwa sipendi kununua chakula kazini---kama unavyona hapo ndo mlo umekamilika nitakula leo jioni niwapo kazini ...JUMATATU NJEMA KWA WOTE.

16 comments:

Emmanuel Mhagama said...

Dada kwa mtindo huu wa kutamanishana siku nyingine nitakudai unitumie kwenye e-mail as an attachment, ha ha ha ha ha. Inaonekana Jumapili ilikuwa nzuri sana, nimetamani kama ningekuwepo vile na mie "nipochoe". Wacha ninywe maji nishushie haya mate. teh teh teh teh!!

sam mbogo said...

chakula kitamu umepika. hongera kwa kupata muda wa kufanya hivyo.kwa maana hiyo kilicho baki jana unakila leo kama KIPOLO??.haya kazi njema DA YASINTA. kaka s

Anonymous said...

Kumbe ni mpishi mzuri sana, sasa itabidi nikaribie kwako Yasinta, kwa chakula hicho hicho. Mh! nimekipenda sana ila ukiweza unipikie na chapati zakukanda. Siku njema.

Yasinta Ngonyani said...

Kaka yangu Mhagama wenga nywi tu maji ago kuhelelesa ..usipate shida karibu kipo kwa ajili yako pia

Kaka Sam Yaani kama ulikuwepo kilikuwa bongo la utamu..KIPOLO hahahaaaa kaaazi kwelikweli

Usiye na jina! Umenichekesha kweli kupika nilianza nikiwa na miaka mitano. Hakuna shida ww karibu sana na wala usikonde chapati utapata ..siku njema nawe pia ila ningefurahi kujua jina lako...kupata mgeni bila kujua jina kweli???

Anonymous said...

Yani asiye na jina huyu, ndiye huyohuyo uliyemuuliza jina kwenye ile habari ya wanawake wanao onewa ruhuwiko, sijapata mda wa kukupa jina langu ila utalijua tu.

isaackin said...

Safi sana msosi unavutia

Rachel Siwa said...

Mmmhhh tamu saana..Hongera kwa mapishi KADALA..

Yasinta Ngonyani said...

Oh! kumbe ni wewe usiye na jina ..haya ntafurahi sana kukufahamu....
Kaka Isaack! sio kuvutia tu ulikuwa mtamu sana pia:-)

KACHIK! YAANI SI UWONGO ULIKUWA MTAMU MNO ..AHSANTE kwa hongera...

Salehe Msanda said...

Habari.
Hongera kwa kujali afya

Kila la kheri

Interestedtips said...

mweh mweh.......mbona njaa imeumaaaaaa

ray njau said...

Asante sana kwa mlo mzuri na yenye kuzingatia viwango na masharti ya tasnia ya mapishi.

Yasinta Ngonyani said...

Kaka Salehe! Afya ni muhimu katika maisha..ahsante kwa mchango wako.

Ester! nakuambia chakula kilikuwa kitamu si mchezo siku tukikutana ntakupikia kama hiki najua utakipenda...pole kwa kuwa na njaaaa baada ya kuona makulaji haya...

Kaka Ray...Mwanamke na mapichi si ndio:-)

Mija Shija Sayi said...

Yasinta imebaki kuanzisha Restaurant tu...

Unasubiri nini?

Yasinta Ngonyani said...

Mija Mija Dada msaidizi...oh ni dada msaidizi kwa maana hiyo utakuja kunisaidia dada mkuu au sio?

Kajunason said...

Dah! umenitamanisha sana... Udendaaaaa

Yasinta Ngonyani said...

Shem Cathbert! karibu sana hapa kibarza cha maisha na mafanikio..na pole kwa kukutamanisha ila karibu ushiriki nasi:-)