Friday, May 14, 2010

Ujumbe wa Ijumaa ya leo!!

Hata kama ukiamua kutoka kwenye
ndoa ngumu huna haja ya kujilaumu.

Maishani ukiwa mtu mwenye kukubali kwamba chanzo cha tatizo ni wewe hutapata shida na tena utazidi kujiimarisha kwani hakuna apendaye kulaumiwa duniani na kumbuka kwamba jamii yetu imefunzwa kwamba kukosea ni ujinga. Kumbe pia inapaswa kufunzwa kwamba kukosea -ni elimu kama unayatumia makosa vizuri. Na zaidi ya yote tukumbuke ya kwamba lawama si mzigo. Kama unapenda usawa, upendo na haki usiogope lawama haitakuumiza popote. ...........Huu ndio ujumbe wangu wa IJUMAA YA leo......IJUMAA NJEMA KWA WOTEEEEEEEEEEEE

6 comments:

Fadhy Mtanga said...

Ijumaa njema nawe pia.

Koero Mkundi said...

NI UJUMBE MZURI DADA, DAIMA HUWA TUNAJIFUNZA KUTOKANA NA MAKOSA. NA NDIO SABABU TUNAAMBIWA KUWA NI BORA UJARIBU UKOSEE KULIKO KUACHA KABISA....KWANI KATIKA KUKOSEA HUKO KUNA KUJIFUNZA PIA.....

NAKUTAKIA SIKU NJEMA WEWE NA FAMILIA YAKO

o'Wambura Ng'wanambiti! said...

aksentiii!

PASSION4FASHION.TZ said...

Nawe pia pamoja na familia kwa ujumla.

Baraka Chibiriti said...

Asante sana Dada Yasinta kwa ujumbe mzuri,

Ijumaa njema nawe pia na familia yako.

Anonymous said...

upate siku njema