Wednesday, May 5, 2010

KUPENDA NI NINI? KUMBUKUMBU YA MUNGA TEHENAN SEHEMU YA PILI!!

Ilipoishia…….
Bila shaka huwa unakutana na vitukovya karne kila siku kuhusu jambo hili. Mtu anaambiwa na mwingine kwamba hampendi. Inawezekana kuwa ni wapenzi wa muda mrefu-mke na mume au hata wa muda mfupi. Badala ya huyu anayeambiwa huapendwa kukubali jambo hilo kwa sababu hawezi kulibadili, kupinga. Wengine huenda hata mahakamani au kuwauwa wapenzi waliowakataa. Inaendele…..


Vituko hivi viko hata katika mazingira ambapo hakuna ugomvi au kutoelewana. Inawezekana ni katika mazingira ya kawaida kabisa, ambapo mpenzi anamuuliza mwenzake , ”hivi, unanipenda kweli, hebu nithibitishie”
Shabashi! Ni kitu gani hiki! Tangu lini kupendwa limekuwa ni jukumu lako? Jukumu lako ni kupenda, basi. Hili jukumu la kupendwa muachie mwingine.
Kupenda ni hisia na ndiyo maana imekuwa vigumu sana kwa watu kumudu kusema mapenzi ni nini. Jambo loloto la kihisi ni gumu kuelezewa kwa maneno. Kupenda kunapoelezeka kwamba ni kitu fulani, ni lazima kuna mushkeli.
Watu wengi ambao huwa ninazungumza nao katika kushauriana au kufundishana kuhusu kupenda, huwa ninawauliza swali hili ”Umempendae kitu gani mwenzako?” Wengi huwa wanatoa maelezo kama vile, ”nimempendea upole wake” au ”nimempenddea ukarimu wake” ama ”nimempendea tabia yzake”.

Lakini hakuna kabisa ambao wamewahi kusema wamempenda mwingine kwa sababu ya sura au maumbile yao au kwa sababu ya utajiri ama umaarufu wao . Kwa nini?
Ni kwa sababu, ndani ya nafsi zetu tunajua kwamba kupenda sifa za nje ni jambo linalopingwa na kila mtu n ani aibu kulitamka, labda tu miongoni mwa watu waliozoeana sana na kuaminiana.
Hata hivyo, miongoni mwa wapenzi, jambo hilo huwa linasemwa sana bila wenyewe kungámua. ”Unaniacha hoi kwa macho yako,” ni kauli za kawaida kwa wapenzi. Kusikia mpenzi akimwambia mwingine ”nimekupenda kwa kweli, guu unalo,” ni jambo la kawaida.
Mwanamke na kuita hali hiyo kuwa ni kupenda. Hutamani sana sura, miguu, matiti, makalio, macho na hata midomo n apua. Hili ni jambo la kimaumbile zaidi. Ndiyo maana wanawake wanajipamba na kujikwatua. Hufanya hivyo ili kuwavuta wanaume, kwani wanaume hujali muonekano wa nje zaidi.

Kuna wakati hapa nchini suala la wanawake kubabua ngozi au kupaka dawa nywele zao lilikuwa ni suala la mjadala mkubwa. Baadhi ya wanawake ambao walitakiwa kutoa maoni yao kuhusu jambo hili walisema, wao hawapendi sana kufanya hivyo, bali wanaume ndiyo wanaowalazimisha kufanya hivyo.
”mwanaume anaweza kukuacha kwa sababu tu kaona mwingine mwenye ngozi nyeupe na nyororo au nywele laini zilizoangukia mabegeni. Inabidi ujitahidi kumlinda.” walisema , baadhi ya wanawake. Pamoja na kuwa ni kauli zenye kuonyesha unyonge, lakini zina ukweli. Wanaume hukimbilia sifa za nje zaidi.

Wanawake kwa upande wao, huvutwa zaidi na wanaume ambao wanaweza kuwalinda au kuwapa uhakika fulani wa kimaisha. Hata hivyo, unapowauliza kwa nini wamempenda fulani, nao hawawezi kusema ni kwa sababu an fedha au kwa sababu ana jina, hapana. Ni aibu kukiri hivyo au pia kwa sehemu kubwa huwa hawajui kwamba wamevutwa na sifa hizo.
Ni wachache sana ambao hutokea wakajibu kwamba wamempenda mwingine kwa kumpenda tu, bila kutoa maelezo. Kwa nini ni wachache? Ni kwa sababu, wanaopensa siyo wengi. Mtu anayesema nimempenda fulani bila kujua ni kwa nini hasa, huyu ndiye ambaye amependa. Huku ndiko tunakoita kupenda tunapopenda, kwa kawaida kuwa hatuju sababu za kumpenda huyo fulani, bali tunampenda tu. Mtu anapotoa sababu ya kumpenda mwingine, huyo hajapenda bado. Huu ndiyo ukweli!

Kwa bahati mbaya, kuna wengine wamependa na hawajui ni kwa nini wamependa. Lakini unapowauliza, wanaanza kujaribu kutafuta sababu za huko kupenda kwako. Kwa hiyo, mtu ataanza kusema, `nampendea upole`au `nampendea huruma zake` ama `nampenda kwa sabu ametulia.” Anasema haya kwa sababu anaamini kwamba, kupenda ni lazima kutolewe sababu, wakati kinyume chake ndiyo ukweli.

Unapovutwa na mtu na ukajikuta huna sababu unazoweza kuzitoa za kwa nini umevutwa naye, kuna uwezekano mkubwa kwamba uko kwenye upendo wa kweli na mtu huyo. Lakini pale ambapo unaziona sababu waziwazi za kumpenda kwako, hapo hakuna upendo wa kweli.
Kumbuka kuwa sababu zote unazoziona ni za muda, zinaweza kuondoka. Zinapoondoka, ina maana pia kwamba, upendo haupo. Kama ulimpenda kwa sababu ya tabia ya upole na ukarimu, anapokuja kubadilika na kuiacha tabia hio, itakuwa na maana pia kwamba, mapenzi hayatakuwepo kwani ulichokipenda kitakuwa hakipo.

Lakini ukiona mwingine mwenye upole na ukarimu kuliko huyo, utampenda zaidi pia. Je, utaacha kumpenda yule wa kwanza au utawapanga kwa madaraja kiupendo?
Kama ulimpendea sura, mguu au jicho, ni wazi upendo wenu utakuwa ni wa muda kwani kwa kadiri siku zinavyopita, vitu hivyo havyo hupoteza nuru na mvuto. Mazoea nayo huingiza ukinaifu wa hisia. Lakini kuna wengine ambao wana miguu na macho mazuri zaidi ya hayo ya huyo. Hii ina maana kwamba, utahama kutoka mtu mmoja hadi mwingine ukifuata uzuri.

Kumpenda mtu bila kujua ni kwa nini umempenda, kuna maana ya kumkubali mtu huyo kama alivyo, kumpokea bila masharti. Kuna maelezo na nadharia nyingi zenye kuonyesha ni kwa nini siyo kila mtu anaweza kumpenda mwingine kwa njia hii.
Lakini bila shaka, nadharia na maelezo hayo hayana nafasi kubwa sana kwetu katika kujadili jambo hili. Chenye nafasi, ni kujua namna mtu anavyoweza kupima aina ya mapenzi aliyomo. ….tutaendelea wiki ijayo.

Habari hii ni kutoka kitabu cha MAPENZI kuchipua na kuchanua kilichoandikwa na MUNGA TEHENAN



Sio mbaya kama tukimsikiliza dada Saida Karoli na wimbo wake wa Mpenzi nakupenda

1 comment:

MARKUS MPANGALA said...

Ni kupenda kusiko na sbabu, lakini ukitoa sababi basi hupendi. Je ile sababu siku hiyo ikikosekana, utafanyaje? Mapenzi ni safi ukipanat akupendaye. Mapenzi matamu ukifarijika kumpata akifarijiye. Hakika mapenzi ni muamana hata maualana anajua hilo.

Baada ya MUNGA TEHENAN soma na mashairi ya Profes Zakaria Mochiwa ktika MVUMILIVU HULA MBOVU. ni mapenzi makali na yenyeb utamu na uchungu kwa mashairi yenye ladha