Monday, May 31, 2010

BLOG YA WASIOONA YAANZISHWA:- TANZANIA LEAGUE OF THR BLIND TEMEKE DISTRICT

Umoja ni nguvu


Ulimwengu wa Bloggers sasa unazidi kupanuka, kwani wasioona Wilaya ya
Temeke “Tanzania League of the Blind Temeke District nao wameamua
kufungua Blog yao.

Akiongelea Blog hiyo Mwenyekiti wa Chama hicho ndugu Abdala Ally
Nyangalio alisema kufunguliwa kwa tovuti hiyo ndogo kumekuja baada ya
chama hicho kupata mafunzo ya Utawala bora ambapo moja ya masomo
waliyojifunza ni matumizi ya TEHAMA (ICT) katika maendeleo.

Katika mafunzo hayo yaliyofadhiliwa na Foundation for Civil Society,
Washiriki wa semina hiyo walivutiwa sana na somo hilo na kuomba
ushauri na msaada zaidi kutoka kwa mwezeshaji Ndugu. Jacob Malihoja
ambaye hakusita kuwasaidia kufungua tovuti ndogo (Blog) hiyo.

Akielezea zaidi Bw. Nyangalio alisema kuwa madhumuni ya kufungua
tovuti hiyo ni kuweza kupata mawasiliano na watu ama taasisi mbali
mbali wenye moyo wa ubinadamu, moyo wa huruma kwa walemavu ili waweze
kutoa mchango wao kuwasaidia walemavu wasioona wilaya ya Temeke kila
mmoja kwa kadiri ya nafsi aliyonayo.

Ndugu Nyangalio pia alisema kupitia Blog hiyo wataweza kupata mawazo
na maoni mbali mbali kutoka kwa watu wenye moyo na nia njema katika
kufanikisha harakati zao mbali mbali walizonazo na watakazokuwanazo.

Mwezeshaji huyo waliyemtaja ambaye ni Blogger mwenzetu Ndugu Jacob
Malihoja, alisema kuwa ndugu hawa wanahitaji kusaidiwa kila mmoja kwa
kadiri ya uwezo na nafasi aliyonayo ya kuwasaidia.

Aidha ndugu. Malihoja alisema anawashauri watu mbali mbali
watakaotembelea blog hiyo wawasiliane na viongozi wa Chama hicho
ikiwezekana kwa simu na kuwatia moyo katika juhudi walizonazo kwani
alichojifunza ni kuwa wanahitaji sana kutiwa moyo jambo ambalo
linawaongezea moyo na kasi ya kujiinua na kushiriki katika maendeleo
ya Taifa.

Sambamba na hilo Ndugu Malihoja alisema yeyote mwenye uwezo wa
kujitolea kuwasaidia katika harakati zao, yeye mwenyewe au
kuwaunganisha na watu wanaoweza kuwasaidia litakuwa ni jambo bora sana
kufanya hivyo.

Bw. Nyangalio pia alisema blog hiyo itakapokuwa kanmilika kwa kuwekwa
taarifa zote muhimu wanazohitaji watafanya sherehe ya uzinduzi katika
tukio litakalohusisha wasioona wote Wilaya ya Temeke, Viongozi wa
Serikali na kisiasa, wafanyabiashara na wadau wengine mbali mbali
wataalikwa.

Zaiai ingia hapa kuwasoma http://www.tlbtemeked.blogspot.com/

2 comments:

Penina Simon said...

Thanks to lord, nao wanatakiwa wapewe nafasi kwani wanaweza.

Yasinta Ngonyani said...

Napenda kuwakaribisheni katika ulimwengu huu wa kublog sisi sote ni ndugu, watoto wa baba mmoja. Upendo Daima.