Wednesday, July 2, 2014

PALE INAPOTOKEA KUPEANA HABARI KUNAPOKOSEKANA NA PALE PANAPOKUWEPO KUPEANA HABARI KWA WANANDOA....

MAISHA YA NDOA YA YOSEFU NA PAULINA...
Walikuwa katika hali ya uchumba kwa mwaka mzima sasa. Kwa muda wa miezi sita walikuwa wakionana karibu kila siku. Lakini baada ya hapa, Yosefu aliondoka kwenda kutafuta kazi nzuri. Mwanzoni alimwandikia barua Paulina mara kwa mara. Lakini muda kidogo, barua zilianza kupungua na zile alizopata Paulina hazikuwa na maneno ambayo alitazamia yawemo. Yusefu aliongelea machache sana kuhusu maisha ya mjini, na alisema kidogo tu kuhusu kazi yake mpya na rafiki zake wa huko.
Paulina alianza kupatwa na wasiwasi, kwa kweli wasiwasi mwingi. Lakini hakumwambia Yosefu. Mwanzoni alikuwa anamwandikia juu ya yale mambo aliyopenda na Yosefu ni mzima na angelikuja kumwona hivi karibuni. Lakini mara aliacha kutaja mambo haya. Aliongea tu juu ya mambo ya kijijini na matukio yaliyotukia hivi karubuni katika parokia yao. Zaidi kuhusu mwenyewe hakusema tena.
Kadri miezi ilivyopita ndivyo moyo wake ulivyozidi kujawa na uchungu na bumbuwazi. Angewezaje kuzungumza juu ya mambo yake binfsi kama Yosefu alikuwa hatilii maanani mambo haya? Bada ya miezi sita Yosefu alirudi nyumbani kwa likizo la majuma matatu. Alishangazwa na hata kushtuka kuona jinsi Paulina alivyokuwa hamjali.






























Wazo na swali kutoka kwa Kapulya wenu:- "Na ndio maana kupeana habari ni muhimu kwani mwenzio hawezi kujua wewe unawaza nini na wewe huwezi kujua wenzio anawaza nini.
Na sasa hata  Yosefu anausikitikia mwenendo wa Paulina. Je? watafanya nini?...unfikiri ikiwa wataongelea waziwazi juu ya tatizo lao mapenzi yao yaweza kufufuka?  "  Halafu leo ni tarehe ambayo nilifunga pingu za maisha na baba watoto:-)

CHANZO :- KITABU NJIA YETU KWA MAPENDO NA NDOA

4 comments:

emu-three said...

Mawasiliano katika ndoa ni muhimu sana, kuambizana ukweli, kusiwe na usiri usiri, maana wanandoa ni kitu kimoja, kwann sasa kuwe na kufichana, hapo ndio mwanzo wa kumegeka kwa mshikamano wa ndoa, na ndoa kuwa kama ubia 2
Tupo pamoja ndugu wangu

ray njau said...

Imarisha Ndoa Yako Kupitia Mawasiliano Mazuri
---------------------------
“Neno linalosemwa wakati unaofaa ni kama matunda ya mtofaa ya dhahabu kwenye chombo cha fedha kilichopambwa.” —MET. 25:11.

Je, wewe na mwenzi wako wa ndoa mna mawasiliano mazuri, au mnashindwa kufanya hivyo? Bila shaka, matatizo yanaweza kutokea kwa kuwa ndoa inawaunganisha watu wawili wasio wakamilifu, wenye nyutu na tabia tofauti zinazotegemea utamaduni na malezi yao. (Rom. 3:23) Isitoshe, huenda njia ya mume ya kuwasiliana ikawa tofauti na ya mke wake. Ndiyo sababu watafiti wa ndoa John M. Gottman na Nan Silver wanasema hivi: “Wenzi wa ndoa wanahitaji kuazimia, kuwa na ujasiri na uvumilivu ili kuwa na uhusiano wenye kudumu.”

Ni muhimu kwa mume na mke kusali na kutamani sana kuboresha ustadi wao wa kuwasiliana. Ni kweli kwamba inaweza kuwa vigumu kuacha mazoea ya zamani. Lakini mume na mke wanapompenda Yehova, wanapomwomba awape roho yake, na kuona muungano wao kuwa mtakatifu, wanachochewa zaidi kufanya mabadiliko na hivyo wanakuwa tofauti na wenzi wengi wa ndoa. Mke aliyeolewa kwa miaka 26 aliandika hivi: “Mimi na mume wangu tunachukua kwa uzito maoni ya Yehova kuhusu ndoa, kwa hiyo hatufikirii kamwe kutengana. Hilo linatufanya tujitahidi zaidi kutatua matatizo kwa kuyazungumzia pamoja.” Ushikamanifu na ujitoaji huo wa kimungu humpendeza Mungu na huleta baraka nyingi.—Zab. 127:1.

KUENI KATIKA UPENDO

Upendo, “kifungo kikamilifu cha muungano,” ndiyo sifa muhimu zaidi katika ndoa. (Kol. 3:14) Upendo wa kweli hukua kati ya wenzi wa ndoa washikamanifu kadiri wanavyoendelea kuishi pamoja, kukabiliana na matatizo, na kufurahia baraka pamoja. Urafiki wao unakuwa wa karibu hata zaidi na wanafurahia sana kuwa pamoja. Ndoa za aina hiyo hazijengwi kwa matendo machache tu ya pekee kama inavyoonyeshwa katika vyombo vya habari, badala yake zinajengwa kwa matendo mengi sana madogo-madogo, kama vile kukumbatia, kusema neno la fadhili, tendo linaloonyesha unajali, tabasamu changamfu, au kuuliza hivi kwa unyoofu, “umeshindaje?” Mambo hayo madogo-madogo yanaweza kuboresha sana ndoa. Mume na mke ambao wamekuwa na ndoa yenye furaha kwa miaka 19 hupigiana simu au kutumiana ujumbe mfupi ili “kujuliana hali,” akasema mume.

Upendo humchochea pia mume au mke kuendelea kumjua mwenzi wake. (Flp. 2:4) Ujuzi huo hufanya upendo wao uimarike hata zaidi licha ya kutokamilika kwao. Ndoa yenye mafanikio haibaki palepale, badala yake inakua na kuimarika zaidi kadiri wakati unavyopita. Kwa hiyo, ikiwa umefunga ndoa, jiulize: ‘Ninamjua vyema kadiri gani mwenzi wangu? Je, ninaelewa hisia na maoni yake kuhusu mambo? Mimi humfikiria mwenzi wangu mara nyingi kadiri gani, labda nikitafakari sifa zake zilizonivutia mwanzoni?’

ONYESHA UNYENYEKEVU WA KWELI
Mawasiliano mazuri katika ndoa ni kama kijito cha maji kinachotiririka polepole kwa utulivu kwenye bustani. Ili kijito hicho kiendelee kutiririka, ni muhimu sana kuwa “wanyenyekevu katika akili.” (1 Pet. 3:8) Ndugu mmoja ambaye ameoa kwa miaka 11 alisema hivi: “Unyenyekevu ndiyo njia ya haraka zaidi ya kusuluhisha hali ya kutoelewana kwa kuwa unyenyekevu unakuchochea kusema, ‘Pole.’” Mzee mmoja ambaye kwa miaka 20 amekuwa na ndoa yenye furaha alisema: “Nyakati nyingine neno ‘Pole’ ni muhimu zaidi kuliko neno ‘Ninakupenda.’” Aliongezea hivi: “Sala ni kati ya njia za haraka zaidi zinazomsaidia mtu kusitawisha unyenyekevu. Mimi na mke wangu tunapomfikia Yehova pamoja katika sala, tunakumbuka hali yetu ya kutokamilika na fadhili zisizostahiliwa za Mungu. Kukumbuka mambo hayo muhimu hunisaidia kuwa na maoni yanayofaa.”(Kutoka maktaba:www.jw.org)

ray njau said...

SITAWISHA HESHIMA

11 Hata ndoa zenye furaha zaidi si kamilifu, na mume na mke wanaopendana hukosa kuelewana nyakati nyingine. Abrahamu na Sara hawakukubaliana kila mara. (Mwa. 21:9-11) Hata hivyo, tofauti hizo hazikuwatenganisha. Kwa nini? Walitendeana kwa staha na heshima. Kwa mfano, Abrahamu alimwambia Sara “tafadhali.” (Mwa. 12:11, 13) Naye Sara alimtii Abrahamu na kumwona kuwa “bwana” wake. (Mwa. 18:12) Ikiwa mume na mke hawaheshimiani, kwa kawaida hilo litaonekana wazi kupitia maneno au sauti yao. (Met. 12:18) Wasipotatua tatizo lenyewe, huenda ndoa yao ikawa hatarini.—Soma Yakobo 3:7-10, 17, 18.

12 Wale waliofunga ndoa karibuni wanapaswa hasa kujitahidi kuzungumza kwa fadhili na heshima ili iwe rahisi kwao kuwasiliana waziwazi na kwa unyoofu. Mume mmoja anakumbuka hivi: “Ingawa miaka ya kwanza ya ndoa ni yenye shangwe, nyakati nyingine inaweza kuvunja moyo. Unapojaribu kuelewa hisia, tabia, na mahitaji ya mke wako, na mke wako anapojaribu kukuelewa, mambo yanaweza kuwa magumu! Hata hivyo, mambo yanaweza kuwa rahisi zaidi mkiwa na usawaziko, ucheshi, na sifa zinazoimarisha ndoa, yaani, unyenyekevu, subira, na kumtegemea Yehova.” Hilo ni jambo la kweli kabisa!

Yasinta Ngonyani said...

Ahsanteni kwa kupita hapa na kuacha machache mazuri yaliyo mayoni mwenu.

Kipeana habari kunspokuwepo....vizuizi vyenye kuleta utengano kati ya watu wawili huvinjika, badala ya kujisikia pekee watu hawa wawili wanaelekea maisha ya kutoa nakupokea, kunakuwa na hisi mpya ya umoja, tofauti kati yao husawazishwa kwa urahisi, mahitaji ya kila mmoja wao yaonekana na kutimizwa na pia kinakuwa na hali ya kujenga kitu kwa pamoja.