Tuesday, October 8, 2013

HIVI NDIVYO MAPISHI YA NANGONYANI YALIVYOKUWA JANA JIONI SAMAKI WA KIHINDI!!!

 Hapa samaki anaandaliwa, ni samaki wa kihindi inaitwa KHARI MACHLEE  ulikuwa mlo wangu wa jana jioni unaweza kula na wali, ugali na mikate pia.
Na hapa ndo tayari ameiva na tayari kwa kuliwa ni mlo mzuri kwa kweli ...nilipitiwa kwa utamu nikasahau kupiga picha ilivyokuwa kwenye sahani yangu ilivyoonekana...:-) Kapulya

5 comments:

ray njau said...

Kwa kweli ni mlo wenye hadhi kamili kwa ladha maridhawa iliyohanikizwa na harufu yenye mvuto kwa walaji na familia!!Hongera sana!!

Anonymous said...

Da Yasinta, huo mchuzi mwekundu sana nadhani tomato zako zote za shambani umezimalizia hapo. Vipi ulisema utanitumia email, kimya tuu. By Salumu.

Yasinta Ngonyani said...

Ndugu yangu Ray! ni kweli chakula kilikuwa na ladha na harufu mpaka kilipoteremka tumboni...

Kaka Salumu! Hahahaaa umenichekesha kweli ..hapana nyanya bado zipo na wala usiache kuja kula

Anonymous said...

Jamani jamani hicho chakula jamani! Huyo samaki nibakishie kipande change kwa kweli na rosti yake, sijui ulikula na wali au mkate? ukiweza unipostie kwa anwani ile ile. Siku njema.

Yasinta Ngonyani said...

Usiye na jina wala usikonde samaki yupo njiani..mimi nilikula kwa wali..