Friday, October 11, 2013

NAPENDA KUWATAKIENI WOTE MWISHO WA JUMA MWEMA NA PIA IJUMAA NJEMA SANA!!!

Leo nasema tu Ijumaa iwe njema sana maana ndio mwanzo wa mwisho wa juma hili. Walio na familia basi wajaribu kuwa na familia, na pia ni safi ukawa na rafiki , jirani ni muhimu katika maisha kubadilisha mawazo.

Ujumbe mdogo wa Ijumaa:- Dunia ni kama kitabu, na wale ambao hawasafiri, wanasoma ukurasa mmoja tu.
IJUMAA NJEMA NDUGU ZANGUNI!!!

3 comments:

ray njau said...

Ni hakika na kweli mdada wa kindendeule ........!Kutoka kwenye ardhi ya wandendeule kwa mzee Dadi Nyongani hadi kwenye ardhi ya waswidi ni milima na mabonde na umejonea mengi katika kazi ya muumba wetu mtukufu na utkufu wake kule mbinguni.
"Hakika mtembea bure siyo sawa na mkaa bure maana hukutana na vya bure katika mapito yake".

Anonymous said...

Ijumaa njema kwa wote, na nawatakia sikukuu ya EID EL ADHA kwa wote ambayo itaangukia siku ya Jumanne ijayo.

Anonymous said...

Nimeipenda sana hii nanukuu`Dunia ni kama kitabu, na wale ambao hawasafiri, wanasoma ukurasa mmoja tu`. ni kweli kabisa ili usafiri na inabidi kusoma kitabu chote. Ubarikiwe sana Yasinta kutupatia mambo mapya kila wakati.