Friday, December 30, 2011

Wanawake hukubali kufa huku wakiona......!

Tunajua wote kwamba, hutokea wanawake wakateswa sana kwenye uhusiano wao wa kindoa au kimapenzi na bado wakaendelea kukaa tu kwenye uhusiano huo. Inafikia hadi mtu anakufa huku akiona kabisa. Watu wengine huiita hali hii kuwa ni ujinga na wengine huita kulogwa au huelezea hali hii kwa njia ambayo haiwapi haki wanawake hao. Zipo sababu nyingi ambazo zinawafanya wanawake kuendelea kukaa kwenye ndoa ngumu, bila hata kufikiria kuondoka. Sababu nyingine zinaweza kuonekana kama kituko, lakini ndizo zinazowafanya wafie kwenye ndoa.Kuna ile sababu kwamba, hawajui ukubwa wa kiwango cha mateso. Hii hutokana na kwamba, baada ya kuzoea mateso, mwanamke hufikia kuamini kwamba, hayo siyo mateso, bali ndivyo ndoa inavyotakiwa iwe. Kuna sababu ya kukosa marafiki, ndugu au jamaa wa karibu. Na kwa sababu hana watu wa aina hiyo, inakuwa vigumu kwake kuwa na mahali pa kukimbilia ili aweze kupata nafasi ya kujiandaa kuanza upya maisha.Kuna wanaoendelea kukaa kwa sababu dini zao zinawaambia, hawana budi kukaa, kwani wameshakuwa mwili mmoja na waume zao na hivyo hawawezi kuondoka. Wanafikiria iwapo wataamua kutoroka, viongozi wao wa dini watawaona vipi na waumini wenzao watachukuliaje jambo hilo. Kwa hiyo, wanaishi kwenye ndoa hizo kwa sababu ya dini, siyo kwa sababu yao binafsi. Halafu kuna suala la kupenda. Utegemezi wa kihisia huwa unaitwa kupenda. Kwa hiyo mwanamke anasema anampenda fulani kiasi kwamba, hawezi kumwacha, wakati ukweli ni kwamba, anamtegemea mwanaume huyo kihisia.Wanawake wanaoteswa kwenye ndoa, huwa wanajidanganya kwamba, watamudu siku moja kubadili tabia hiyo a waume zao kuwafuja. Wanajiambia kwamba, kutukanwa, kupigwa, kudhalilishwa, na matendo mengine, siyo hiari ya hao waume wao. Hivyo wanaamini kwamba, kuna siku watamudu kuwasaidia watoke kwenye tabia hizo. Lakini wakati mwingine wanaume hawa watesaji, huwa wanajidai kusema kwamba, wanafanya mambo hayo bila kujua sababu na kuna wakati wanasema wamelogwa.Hujawahi kuwaona wanawake wanaokwenda kwa waganga kutafuta dawa ili waume zao wasiwapige, ati kwa sababu vipigo vyao vinatokana na kuchananywa na uchawi wanaofanyiwa na wanawake zao wa nje? Mwanamke anaamini kabisa kwamba, mumewe hamjali na anamdhalilisha kwa sababu ya kulogwa!Mwanamke anaweza kujiambia kwamba, kwa sababu mume wake kuna wakati anamtendea wema, hata kama ni moja, basi anampenda na hayo mengine mabaya, yatakwisha au ni bahati mbaya. Mwanamke pia anaweza kufikiri kwamba, akijitahidi sana kumfurahisha mumewe, mume huyo atabadilka na kuwa na tabia nzuri. Hivyo hujipendekeza na mwanaume habadiliki na mateso yanaongezeka. Kuna wanaomudu kuishi kwenye uhusiano huu wa sababu, wamemudu kukandamiza, kupunguza ukubwa wa maumivu. Wanajiambia kwamba, wanavyotendewa siyo vibaya sana. Mwanamke anaweza kujiambia, ‘alinipiga kidogo tu, tena mara mbili kwa mwezi, kuna wanaopigwa kila siku.’ Huyu amehalalisha kipigo na mateso, hawezi kuondoka.Kuna wanawake wanaoamini kwamba, ndoa inajengwa na kuimarishwa na mwanamke au kuvunjwa na mwanamke pia. Kuna andiko moja katika Biblia hutumiwa sana kuwatisha, linalosema, ‘Mwanamke mpumbavu huivunja ndoa yake kwa mikono yake mwenyewe.’ Kwa hiyo wanapofikiria kuondoka, hufikiria kwamba, watu watajua na kumzonga au kumdharau kwa sababu ameshindwa kulinda ndoa. Wengine ni woga tu, kwamba, wakiondoka waume zao watawalipizia visasi au watawasumbua. kuna wakati waume wenyewe ndiyo wanaokuwa wamewatisha kwa kiwango hicho.

**********Nimekutana na hii jamii forum na nimeona si vibaya kama nikiweka hapa...............

3 comments:

ray njau said...

Mwanaume na mwanamke wana wajibu wa pamoja katika kuimarisha kifungo cha ndoa na mpango wa Mungu katika ndoa ni wanandoa waishi pamoja na kujenga familia kwa wakati usi dhahiri.Nje ya hapo ni falsa na nadharia za kilimwengu ambazo hazina nafasi katika mpango wa Mungu.
-------------------------- Ndoa na iheshimiwe kati ya wote, na kitanda cha ndoa kiwe bila unajisi, kwa maana Mungu atawahukumu waasherati na wazinzi. Waebrania 13:4---------

ray njau said...

Mwanaume na mwanamke wana wajibu wa pamoja katika kuimarisha kifungo cha ndoa na mpango wa Mungu katika ndoa ni wanandoa waishi pamoja na kujenga familia kwa wakati usi dhahiri.Nje ya hapo ni falsa na nadharia za kilimwengu ambazo hazina nafasi katika mpango wa Mungu.
-------------------------- Ndoa na iheshimiwe kati ya wote, na kitanda cha ndoa kiwe bila unajisi, kwa maana Mungu atawahukumu waasherati na wazinzi. Waebrania 13:4---------

ray njau said...

1. Biblia husema kwamba mume ndiye kichwa cha familia yake. (1 Wakorintho 11:3) Ni lazima mume awe na mke mmoja tu. Wao wapaswa kuwa wameoana ifaavyo kisheria.—1 Timotheo 3:2; Tito 3:1.

2. Mume apaswa ampende mke wake kama vile ajipendavyo mwenyewe. Apaswa amtendee kwa njia ambayo Yesu huwatendea wafuasi wake. (Waefeso 5:25, 28, 29) Hapaswi kamwe kumpiga mke wake wala kumtenda vibaya kwa njia yoyote ile. Badala ya hivyo, apaswa amwonyeshe heshima na staha.—Wakolosai 3:19; 1 Petro 3:7.


Mungu huwatazamia wazazi wawafundishe watoto wao na kuwasahihisha
3. Baba apaswa afanye kazi kwa bidii ili kutunza familia yake. Ni lazima baba awaandalie mke na watoto wake chakula, mavazi, na nyumba. Ni lazima baba aandalie pia mahitaji ya kiroho ya familia yake. (1 Timotheo 5:8) Yeye huongoza katika kusaidia familia yake ijifunze kumhusu Mungu na makusudi Yake.—Kumbukumbu la Torati 6:4-9; Waefeso 6:4.

4. Mke apaswa awe msaidizi mwema kwa mume wake. (Mwanzo 2:18) Yeye apaswa kumsaidia mume wake katika kufundisha na kuzoeza watoto wao. (Mithali 1:8) Yehova humtaka mke ashughulikie familia yake kwa upendo. (Mithali 31:10, 15, 26, 27; Tito 2:4, 5) Yeye apaswa awe na staha yenye kina kwa mume wake.—Waefeso 5:22, 23, 33.