Friday, January 28, 2011

TUSISAHAU UTAMADUNI/NGOMA ZETU ZA JADI-NGOMA YA CHIYODA/KIODA!!!


Hapa ni ngoma ya kioda(chioda). Ni ngoma ya WamaTengo na inachezwa na akina mama, hapa ni kijiji cha Mkinga katika bonde la Hagati-Mbinga. IJUMAA NA MWISHO WA JUMA MWEMA KWA BURUDANI HII!!!

12 comments:

emu-three said...

Kweli tusisahau utamaduni wetu, kwani mkataa utamaduni wake ni mtumwa...step yako weee, one, twoo..come-on'
Nakumbuka wakati nipo shuleni nilicheza ngoma hizi, na jeshini kidogo,,,siunajua tena mambo ya mujibu wa sheria...!

Unknown said...

Kielelezo cha utamaduni ni kama vile ngoma. Nyimbo, ngonjera na mashairi na muziki wa dansi. Ahsante Dada Yasinta kwa burudani njema...!!

Anonymous said...

Aisee,napenda sana hizi ngoma,kwa kweli Wangoni wamepewa kipaji cha kucheza ngoma yao kitu ambacho hata asiyependa ngoma,mara tu atakapotizama ngoma hizo hakika atavutiwa.Hasa zile wanazovaa nguo nyeupe na tai.
Mimi nilikuwa nataka kujua asili ya kabila hili mahsusi, hivi ni kwanini majina mengi yanayotumika yanaendana na wanyama? mfano Mapunda-punda ni mnyama, Ngonyani-nyani ni mnyama na mengine tu, je kuna historia yoye ya majina hayo au ni majina tu hayana maana?
Samahani,nimeuliza kwa nia njema tu.

Anonymous said...

safi sana we kabinti ka kingoni.umenikumbusha ngoma niliyo cheza wakati na maliza chuo,nikichukua ,dance kama somo langu kuu.hapo ilikuwa mtihani wangu wa mwisho.niliifanyia kazi ya ubunifu ngoma ya mganda.ni baadhi za ngoma ninazo zipenda,bila kusahau,lizombe. kaka s.

Goodman Manyanya Phiri said...

PERFECT BEAUTY! BRAVURA!

chib said...

Swaafi sana

EDNA said...

waoooh hiyo imekaa sawa..siku nyinginye nitakulete ngoma ya kwetu uone WAHEHE tunavjua kudua...lol.

Yasinta Ngonyani said...

Edna nitafurahi sana maana naitafuta kweli hiyo. Hivi inaitwaje ni "limbamiza"? au. na nawashukuru wote kwa mchango wenu.

Simon Kitururu said...

Hivi utamaduni NI NINI?:-(

Mbele said...

Dada Yasinta, nimefurahi sana kuangalia hii ngoma ya kioda. Shukrani kwa kuileta hapa.

Kwa wadau wa blogu hii, napenda kusema kuwa hawa ni wa-Matengo, kabila langu. Hapa wanapocheza ni sehemu inayoitwa Hagati, sehemu ambako nimevinjari tangu nilipokuwa kijana. Huyu anayeongea muda wote anaongea kwa lafudhi ya ki-Matengo kabisa. Yaani nimejisikia nyumbani. Ila inaonekana ameonja ulabu wa kutosha :-)

Anonymous said...

I seldom leave comments on blog, but I have been to this post which was recommend by my friend, lots of valuable details, thanks again.

Na Mpangala said...

Mlongo kwa mala nyingine unikumbushi kutali sana, nakumbuka nilikuwa mbinga katikati ya miaka ya 90 nilimtembelea mjomba mateka nikakuta mashindano ya chioda hee apo ilikuwa kazi kweli. nilipotemka nyasa kwa babu mbamba-bay nikakutana na mashindano ya kioda kile cha kinyasha jamani kwakweli nilifaidi sana na nikumbukumbu kubwa sana kwangu. nashukuru sana mlogno kwa kunikumbusha kwa mala nyingine tena. ubarikiwe sana