Friday, July 25, 2014

MSIONE KUADIMIKA NIPO...PIA NIPO LIKIZO MUDA AMBAO NI MZURI KUWA NA FAMILIA...ILA NIPO!!!!

 Samahani kuadimika  ila nipo  kiaina ....
 ..Nipo likizo na nilikuwa nimejificha hapa na kublog ilikuwa ni kaziii kwelikweli. Nilikuwa na wakati mzuri sana na familia pia baadhi ya marafiki.  katika picha hapo unaona kitu fulani ni wanetu  wapo ziwani kuvua samaki...baada ya muda wakarudi na samaki...
...Na ndo ikawa kazi yangu kumtoa samaki magamba. Kwa vile nimekulia samaki hakuwa kazi kubwa na ngungu kwangu.:-)

7 comments:

Anonymous said...

Da Yasinta tumekumisi sana! Hivi hilo ni ziwa Tanganyika? Tufundishe unavyochoma samaki. By Salumu.

Yasinta Ngonyani said...

Kaka Salumu....ahsante nami nimewamiss mno. Hapana si ziwa Tanganyika...kuchoma samaki...ukisha mtoa magamba..unaweka viungo uvitakavyo na halafu kuchoma...usisahsu pilipili

Salehe Msanda said...

Hongera kwa likizo
Kila la kheri na likizo njema

Yasinta Ngonyani said...

Kaka Salehe! Ahsante nawe uwe na siku njema

Manka said...

Likizo njema Dada Yasinta

Yasinta Ngonyani said...

Ahsante dada Manka ....njoo tule ugali na mchicha , figiri na mboga maboga-:)

Manka said...

Dada yangu unanitamanisha natamani ningekuwa karibu,asante sana,jumapili njema