Thursday, September 26, 2013

NIMELAZIMIKA KUVUNA NYANYA ZANGU KWA AJILI YA BARIDI KUWAHI MAPEMA KULIKO MATARAJIO YANGU....

 Hizi ni nyanya zangu ambazo zilikuwa bado kuiva kama mnavyoona ...nimeamka leo asubuhi  nimeshikwa na butwaa nyasi zote zilikuwa nyeupe theruji  kabisa kitu ambacho zikutarajia kwa haraka hivi. Kwa hiyo imenibidi kuzivuna kabla hazijaharibika sana na kuzihifadhi. Vipi SIJUI kwa kweli..Je nikizihifadhi kwenye boxi zitaiva? Maana hapa ni nusu ya tulizokula....
Hahahaaa:-)  na nikaamua nivune tu na vitunguu vilivyobakia ...mkulima wa ajabu anaanza kula kabla hajavuna na sasa vimebaki sita (6) tu....KARIBUNI KUNISAIDIA KULA NYANYA HIZO!!!

8 comments:

ray njau said...

Kaazi kwelikweli,mabadiliko ya hali ya hewa yasiyotarajiwa yanamlazimisha mkulima kula mbegu na kuuza jembe.
Yasinta kazi ya mikono yako ni nzuri na sana na wala usikate tamaa kwa kuwa kule kusini wanasema:"MADENGO NTIMA."

Anonymous said...

Mie ntakuja kula kachumbari mana una nyanya hapo na kitunguu, nitengenezee ili nyanya zipungue. Ukiziweka kwenye box zitaiva haraka halafu zote kwa wakati mmoja! ila huna jinsi uzitoe kabla hazijaiva sana sana, ivisha taratibu ukiweza. Haya mkulima Yasinta kila la heri.

Unknown said...

tushakaribia dada. We andaa pilau na kachumbari..

Yasinta Ngonyani said...

Kaka Ray! Nashukuru kwa kunitia moyo...ila "MADENDO NTIMA" hiyo kama nimeelewa.

Usiye na jina! Kachumbali utaishindwa mwenyewe....na ahsante kwa ushauri . Ntaweka baadhi kwanza nione kama zitaiva.
Kaka wa mimi Mrope....karibu sana tena sana....na wala usikonde vyote utapata:-D

Rachel Siwa said...

Pole KADALA.lakini si haba tumekula mwaka huu..

Anonymous said...

Wauzie watu wa hoteli na migahawa utapata hela. By Salumu.

Anonymous said...

Ah ah ah hoteli na migahawa, kibongo bongo! Sijui kama ni rahisi hivyo kwa ulaya, embu dada yetu Yasinta atuambie. Mana walivyo strict na kujua zimelimwaje nk!!!Si unajua mambo ya afya kwa nje wenzetu makini. Ila sijui kwa Sweden, Ujerumani hauzi kirahisi hivyo. siku njema.

Yasinta Ngonyani said...

KACHIKI..Ahsante alo..Ni kweli ila hata hivyo nasikitika..njoo chukua nawe:-)

Kaka Salumu! :-) Hapa hakuna mambo hayo labda niwape majirani

Usiye na jina! kumbe unaishi Ujerumani mwenzangu..Basi kanuni/sheri ni hizo hizo..Na kwanza kama una kazi nyingine huwezi tu kuanza kuuza kitu bila kuripoti na kupata kibali na mambo mengine mengiiii.