Wednesday, March 6, 2013

NENO LA JIONI YA LEO :- JE WEWE UNASAMEHE?......JE, UNAPASWA KUONA KWAMBA UMEKOSEWA KIMAKUSUDI?

Kuna hali nyingi maishani zinazomfanya mtu akasirike. Tuseme kwamba unaendesha gari, na karibu ligongwe na gari lingine. Utatendaje? Umesoma kuhusu visa vingi vya madereva wenye hasira waliowashambulia madereva wengine. Hata hivyo, ukiwa Mkristo, bila shaka hungependa kufanya jambo kama hilo. Itakuwa bora zaidi kutua kidogo ili kuchanganua mambo. Labda wewe pia una makosa kwa sababu ulikengeushwa na jambo fulani. Au huenda gari la yule dereva mwingine lilikuwa na tatizo. Somo ni kwamba tunaweza kupunguza hasira, hisia za kukata tamaa, na hisia nyingine zisizofaa tukitumia uelewaji, tukiona mambo kwa njia tofauti, na kuwa tayari kusamehe. Andiko la Mhubiri 7:9linasema hivi: “Usiwe na haraka kuudhika katika roho yako, kwa maana kuudhika hukaa katika kifua cha wajinga.” Usione kwamba umekosewa kimakusudi. Mara nyingi, huenda tukafikiri kwamba mtu fulani ametukosea kimakusudi lakini huenda sivyo ilivyo; labda ni kwa sababu tu ya kutokamilika au kutoelewana. Jitahidi kuwa na maoni yenye usawaziko kuelekea matendo unayoona kuwa si ya fadhili, na uwe tayari kusamehe kwa upendo. Utakuwa mwenye furaha zaidi ukisamehe.—Soma 1 Petro 4:8 NA JIONI IWE NJEMA SANA KWA WOTE

8 comments:

ray njau said...

KWA NINI TUNAHITAJI KUWASAMEHE WENGINE?
============================
Ili tudumishe mahusiano yenye amani pamoja na washiriki wa familia, marafiki, wanadamu wenzetu, na Yehova, ni muhimu tuwe tayari kuwasamehe wale wanaotukosea, iwe ni washiriki wa kutaniko la Kikristo au la. Maandiko yanaonyesha kwamba kuwa tayari kuwasamehe wengine hata wakitukosea mara nyingi kadiri gani ni takwa la Kikristo. Ili kuonyesha hekima ya takwa hilo, Yesu alitoa mfano kuhusu mtumwa fulani aliyekuwa na deni.
Mtumwa huyo alidaiwa na bwana wake pesa zinazolingana na mshahara wa siku 60,000,000; hata hivyo, bwana wake alifuta deni hilo. Baadaye, mtumwa huyo alitoka na kumkuta mtumwa mwenzake aliyekuwa na deni lake lililolingana na mshahara wa siku 100 tu. Mtumwa huyo mwenye deni alimsihi sana amwonyeshe subira, lakini mtumwa aliyekuwa amesamehewa deni kubwa aliagiza mtumwa mwenzake atupwe gerezani. Mtazamo huo ulimkasirisha bwana wao. Bwana huyo akamuuliza hivi: “Haikukupasa wewe . . . kuwa na rehema juu ya mtumwa mwenzako, kama mimi pia nilivyokuwa na rehema juu yako?” “Ndipo bwana wake, akiwa na ghadhabu, akamtia [mtumwa asiyesamehe] mikononi mwa walinzi wa jela, mpaka alipe deni lake lote.”—Mt. 18:21-34.
Yesu alifundisha somo gani kupitia mfano huo? Mwishowe alisema hivi: “Vivyo hivyo Baba yangu wa mbinguni atashughulika nanyi pia ikiwa kila mmoja wenu hatamsamehe ndugu yake kutoka moyoni mwake.” (Mt. 18:35) Somo la Yesu ni wazi. Dhambi ambazo tumetenda muda wote wa maisha yetu ya kutokamilika zinathibitisha kwamba hatuwezi kamwe kutimiza viwango vya Yehova. Hata hivyo, yuko tayari kutusamehe na kufuta kabisa dhambi zetu, kwa njia ya mfano. Kwa hiyo, mtu yeyote anayependa kuwa rafiki ya Yehova ana wajibu wa kusamehe udhaifu wa mwanadamu mwenzake. Au kama Yesu alivyosema katika Mahubiri ya Mlimani: “Ikiwa mnawasamehe watu makosa yao, Baba yenu wa mbinguni atawasamehe ninyi pia; lakini ikiwa hamtawasamehe watu makosa yao, Baba yenu naye hatawasamehe makosa yenu.”—Mt. 6:14, 15.

emuthree said...

Kusamehe, ni ucha mungu wa hali ya juu. Na anayesamehe yupo karibu sana na mola wake.

KWA ujumla kila mtu anatenda makosa, na kama vikombe kwenye kabati hamuwezi kuishi bila kugongana, lkn kiubinadamu, na kwa imani safi, ikitokea kosa, mkikogongana, mkisigishana ni vyema kukimbilia kusameheana.

Wapo watu kazi ya kugombanisha, na wanatafuta upenyo mdogo, na kutumbukiza fitina, hawa watu ni majahili, na wanafanya hayo kwa maslahi yao na ndivyo dunia ilivyo. Na nukuu kidogo kwenye kitabu cha imani, aya hii inasema hivi;

"Shikamana na kusamehe na amrisha mema na wapuuze majahili:. (QURAN 7:199)

ray njau said...

Je unasamehe na kusahau au unasamehe lakini kamwe hutasahau??????????

Steven Bulamu said...

Mtazammo mzuri hata hivyo maandiko yana tuasa sammehe saba mara sabini, mtu akikupiga shavu la kulia mgeuzie na la kushoto, hata mm nasemehe

Shalom said...

Jamani mm nasamehe lkn kamwe sitasahau

Yasinta Ngonyani said...

mie nina swali kidogo hapa:- Je utaratibu sahihi wa kumsamehe /kusamehewa kwa mtu aliyekosa ni upi?
1. Mtu aombae msamaha kwanza/atubu ndipo asamehewe?
2. Asamehewe hata pasipo kuomba msamaha au?
3. Vyote viwili ni sawa?

ray njau said...

@Yasinta!!

Kuwa Tayari Kusamehe
========================
Kusamehe ni njia moja ya kuonyesha upendo. (Wakolosai 3:13, 14) Andiko la 1 Wakorintho 13:5 linasema upendo “hauweki hesabu ya ubaya.” Pindi nyingi, Yesu aliwafundisha wanafunzi wake faida ya kusamehe. Aliwahimiza wawasamehe wengine “si, Mpaka mara 7, bali, Mpaka mara 77,” yaani, bila kipimo. (Mathayo 18:21, 22) Aliwafundisha kwamba mtenda-dhambi anapaswa kusamehewa iwapo baada ya kukemewa, anatubu. (Luka 17:3, 4) Hata hivyo, Yesu hakuwa kama Mafarisayo wanafiki waliofundisha kwa maneno tu; alifundisha kupitia mfano wake pia. (Mathayo 23:2-4) Hebu tuone jinsi Yesu alivyoonyesha kwamba alikuwa tayari kusamehe hata wakati rafiki aliyemtumaini sana alipotenda kinyume na matarajio yake.

ray njau said...

Yesu alikuwa na uhusiano wa karibu pamoja na mtume Petro, aliyekuwa mchangamfu na wakati mwingine alitenda bila kufikiri. Yesu alitambua sifa nzuri za Petro, naye akampa mapendeleo ya pekee. Petro, Yakobo, na Yohana walijionea miujiza fulani ambayo mitume wale wengine hawakuona. (Mathayo 17:1, 2; Luka 8:49-55) Kama tulivyotangulia kuona, Petro alikuwa mmoja wa mitume waliokuwa pamoja na Yesu alipoingia ndani zaidi ya bustani ya Gethsemane usiku ambao alikamatwa. Hata hivyo, usiku huohuo Yesu aliposalitiwa na kukamatwa, Petro na wale mitume wengine walimwacha na kutoroka. Baadaye, Petro alionyesha uhodari kwa kusimama nje huku Yesu akishtakiwa kwa uwongo. Lakini, baadaye Petro aliingiwa na woga, naye akafanya kosa zito—mara tatu alikana kwa uwongo kwamba hata hamjui Yesu! (Mathayo 26:69-75) Yesu alifanya nini? Ungefanya nini ikiwa rafiki yako wa karibu angefanya jambo kama hilo? Yesu alikuwa tayari kumsamehe Petro. Alijua kwamba dhambi hiyo ilimsumbua sana Petro. Kwa kweli, mtume huyo aliyetubu ‘alianza kulia.’ (Marko 14:72) Yesu alipofufuliwa, alimtokea Petro, huenda ili kumfariji na kumtia moyo. (Luka 24:34; 1 Wakorintho 15:5) Baadaye, kabla ya miezi miwili kupita, Yesu alimkweza Petro kwa kumruhusu atoe ushahidi mbele ya umati huko Yerusalemu katika siku ya Pentekoste. (Matendo 2:14-40) Na tukumbuke pia kwamba Yesu hakuwawekea kinyongo mitume wake kwa sababu walimwacha. Badala yake, baada ya kufufuliwa, bado aliwaita “ndugu zangu.” (Mathayo 28:10) Je, si wazi kwamba mbali na kuwahimiza watu wawasamehe wengine, Yesu mwenyewe alikuwa mwenye kusamehe?Tukiwa wanafunzi wa Kristo, tunahitaji kujifunza kuwasamehe wengine. Kwa nini? Tofauti na Yesu, sisi si wakamilifu, na ndivyo na wale ambao huenda wakatukosea. Mara kwa mara, sisi sote tunajikwaa katika neno na tendo. (Waroma 3:23; Yakobo 3:2) Kwa kuwasamehe wengine ikiwa kuna msingi wa kuwaonyesha rehema, tunafungua njia ili Mungu atusamehe. (Marko 11:25) Basi, tunaweza kuonyesha jinsi gani kwamba tuko tayari kuwasamehe wale ambao huenda wakatukosea? Mara nyingi, upendo unatusaidia kuachilia makosa madogo-madogo tunayotendewa na wengine. (1 Petro 4:8) Wale waliotukosea wanapotubu kikweli, kama Petro alivyofanya, bila shaka, tungependa kumwiga Yesu kwa kuwa tayari kuwasamehe. Badala ya kuwawekea kinyongo, tunatenda kwa hekima tunapowasamehe. (Waefeso 4:32) Kwa kufanya hivyo, tunachangia amani kutanikoni, na pia amani yetu wenyewe ya akilini na moyoni.—1