Tuesday, December 13, 2011

Hongera kaka John Mwaipopo kwa kuongeza mwaka"!!!

Katika pitapita zangu nimekuta kaka mwaipopo anatimiza miaka leo. Lakini sijui
ni miaka mingapi umetimiza?. Hongora kaka JOHN KWA SIKU HII MAALUMU. Na hapo naona unashereheke kwa ULANZI... tena linusu lizima wewe kaka weweee nakuamini.

6 comments:

o'Wambura Ng'wanambiti! said...

Hongera sana kaka JM!

Naona unakata kiu ili mwaka uwende vema!!!

Goodman Manyanya Phiri said...

John, umekwisha!!!!


Hongera sana!

John Mwaipopo said...

Yasinta umenisurprise kwelikweli

@ Chaha asante sana kwa kunitakia heri ya kukua haraka. jasiri haachi asili, mimi nilisoma iringa kwa hiyo hii maneno siku mojamoja huwa naichangamkia

@ Goodman. asante sana. karibu juisi ya maparachichi na keki ya ngano isiyokobolewa

Yasinta Ngonyani said...

Nimefurahi kuona kaka Chacha na kaka Phiri mmeungana nami katika kumsherehekea kaka John kwa siku yake ya kuongeza uzee.
Kaka John hii ndiyo ilikuwa sababu kukusurprise. Nafurahi kama imekuwa kama ilivyokuwa SURPRISE.JE? UNATAKA KUTUAMBIA NI MIAKA MINGAPI UMETIMIZA..LOL

Mbele said...

Hongera sana Mkuu. Umenikumbusha mbali. Nami nilisoma Iringa, Mkwawa High School, 1971-72, na ni hapo ndipo nilijifunzia kupiga ulanzi. Enzi zile ilikuwa bakuli moja inauzwa thumni, yaani senti 50.

Kila la heri.

Goodman Manyanya Phiri said...

@John Mwaipopo
Nashukuru sana, Shemeji. Mbona mimi nitazidi kushiba tu!!!

Yote unaenikaribisha nimeshawahi kuyaonja na kuyafaidi huko Kijijini cha Mninga (kama umewahi kufika sehemu za kiwanda cha chai Brooke Bond au Unilever Brothers pitia kituo cha Basi Nyololo).

Mke wangu wa kwanza (SeMakafu) ni mwenyeji wa huko (na tumezaa watoto wawili usije kesho kusema Marehemu Phiri hakuniambia la ushemeji)

Lakini mumeninyima mimi shemeji yenu na Mnyasa tena mtani wenu kabisa... nyama tamu kuliko zote....


MBWA!!!!