Tuesday, March 8, 2011

LEO NI SIKU YA WANAWAKE DUNIANI!!!!

Basi ngoja tusikiize ujumbe huu kutoka kwa Mrisho mpoto usemaye KWANI NI YEYE MAMA!!

12 comments:

malkiory said...

Happy women's day.

Baraka Chibiriti said...

Asante sana kwa ujumbe mzuri sana Dada Yasinta. Basi Hongera sana kwa siku ya leo.
Nimeupenda sana wimbo huu.....kwani twuni ni ya nyumbani kwetu kabisa.

Anonymous said...

safi sana.Yasinta,jaribu pia kutafuta wimbo wa zamani kidogo,unaitwa, Wanawake wa Tanzania wazurisana aa.ni wimbo ambao unaonyesha mtunzi ambaye ni mwanaume alivyokuwa na matarajio ya mwanamke huyu wa kutanzania alivyo nathamani kwake.nina uzoefu fulani katika misha haya ninayo ishi sasa,kiasi kwamba nikimwangalia mwanamke wa kitanzania hakika nafarijika kuona sasa hivi anaweza kuthubutu kama mtakatifu Kitururu asemavyo"Nyoko"katika maisha yake.Taratibu ila nyinyi akina,Yasinta,Da Mija,nk ni mfano tosha katika harakati za kujikomboa, kifikra.
msitusahau nasisi wanaume tuna mkono wetu katika kila hatua ya maendeleo yenu.
kaka s.

Fita Lutonja said...

haya nafurahi kwa kunikumbusha kwani nilikuwa nimesahau kuwa leo ni siku ya wanawake.

emu-three said...

Kila-laheri akina mama, sijui kweli mkiikumbuka siku hii mnawawazia akina mama wanaoteseka huko kijijini.
Najiuliza hivi miradi, misaada inayotolewa kwa kuwasaidia akina mama inawafikia kweli walengwa!
Mijini nii kila kitu, nashindwa kuua kwanini sera zisiangalie uwezekanao wa kuboresha vijiji ili watu wasikimbilie mjini, Kwa mfano wawekezaji wapewe kipaumbele cha kuwekeza vijijini. Kwasababu wanawake wanaoteseka wapo kijijini. Na wanaoweza kukimbilia mini wengi ni wanaume.
Vitu kama umeme, maji nk, bajeti ya nchi itizame huko kwanza!
Ni mawazo tu

EDNA said...

WANAWAKE OYEEEE.
TUPENDANE NA TUSHIRIKIANE

Unknown said...

Happy women's day dada Yasinta..wanawake oyeeeeeeeeeeeeee

chib said...

Hongereni akina mama kwa siku yenu. Mnahitaji kujikakamua au kusimama kidete kaatika usawa badala ya kupigania upendeleo

Simon Kitururu said...

Hongereni SANA Wadada, WATOTO wa kike, WAMAMA na wanawake!

Mija Shija Sayi said...

Ni nani kama wanawake?

Wanawake juuuuu!!!

Rachel Siwa said...

Wanawake Tusilale bado mapambano!!!!!!!

Goodman Manyanya Phiri said...

Jogoo, kifaranga na yai mbele za macho kweli kabisa (kama mwanamziki anavyoimba) ni vitu mbali sana.


Lakini tunajuwa kwamba mbegu ni ileile moja. Hata kila unapomtazama funza juwa kabisa kwamba yule ni ndugu yako!

Mwaka huu tena umezuka mzozo mkubwa kwamba: je, sikweli kwamba maisha ya binadamu na vyumbe vyote ardhini "haviendi mbinguni baada ya kufa bali vinatoka hukohuko mbinguni KABLA YA KUZALIWA!"http://www.youngzine.com/article/did-meteorite-seed-life-earth [yaani kwamba uhai wetu wote hapa EARTH umekuja kutokana na jalaba la METEORITE kuingia ardhini kutoka mbinguni miaka ya mamilioni yaliyopita]

Ukweli ni kwamba kama sayansi inazidi kusema uhai wote unao umoja, kwanini sisi wanaume twendelee kuwadharau, kuwanyanyasa na kuwakandamiza wanawake na tena ubavu wetu????