Monday, March 21, 2011

Wanawake! naona urembo kweli kazi he he !

ukitaka kupendeza inabidi kuvumilia...
SRXA anasema****Si urembo ndo sababu ya kulia...ni kwa sababu kapima afya majibu si mazuri.....Ebu angalia na nywele zilivyokatika.

TI anasema****Kanyimwa hela na bwana, sasa anaona uchungu kutumia zake anazobana kwenye bajeti ya mboga!

HK anasema ***hapo ni anajiangalia kwenye kioo kaona hajapendeza kama alivotegemea ndo akaanza kulia..................

KIL anasema******Mie naona kama amelazimishwa kunyolewa kwa nguvu na mkasi.Labda mume ameona urembo wake wa nywele unamtia hasara.

FK anasema*****Huyu lazima kuna kitu kimemuudhi sana huko nyumbani. Sasa ili kujiliwaza kaona akajirembe huko salon.Lakini katikati ya urembo huo mawazo yanamjia anabubujikwa na machozi. Kwani kina dada/mama hili halijawahi kuwakuta?
Kuna siku niliona mama mmoja yuko sehemu na watoto wake wanakula lunch. Kajipamba sana ila alikuwa amevaa miwani ya jua nikadhani ni urembo tu. Kumbe nyuma ya hiyo miwani mikubwa alikuwa kaiva macho kwa kulia.

Akina baba/kaka mnatupeleka pabaya sana mjue!

Oneni sasa! Huo mchozi siyo wa maumivu ya kurembwa wala siyo wa kulazimishwa kunyoa nywele maana hapo naona si mchezo katika hiyo Salon ni salon ya uhakika na bei yake si chini ya 40,000/=

GFKanasema****Huyu kapigwa biti na bwana akanyoe kwasababu amekuwa akitoka akiulizwa anasema alikuwa saloon
WAKATI SI KWELI.
Habari hii nimeipata Jamii Forum!!!

2 comments:

chib said...

Labda macho yaliwashwa na ugolo wa kimasai, kwani wamasai ni watumiaji maarufu wa hiyo kitu, tena kuanzia miaka 20 na kuendelea wanavuta kama kawa

emu-three said...

Hiyo dada yangu inaitwa demohalisia, upendavyo ndivyo iwavyo...! Hata kama hawasemi wewe wahisi ndivyo, nitakiwavyo ili niwe wapendavyo!