Thursday, September 4, 2014

UJUMBE WA LEO kutoka kwa Rais Kikwete "TUTATOA ELIMU YA MSINGI, SEKONDARI BURE"


Katika pitapita zangu jana nikakutana na hii habari/ujumbe kama ni kweli kwa kweli ni habari nzuri sana. Nikaona si vibaya nami nikiiweka hapa Maisha na Mafanikio...Nimeipada hapa haya karibuni tujadili kwa pamoja.
 
Rais Jakaya Kikwete amesema serikali inakusudia kufuta karo kwa wanafunzi wa shule za sekondari za serikali, ili kutoa fursa kwa watoto kusoma bure kuanzia elimu ya msingi, ikiwa ni jitihada za kuinua elimu na kuwapunguzia mzigo wazazi.

“Zipo sababu za msingi zinazosababisha wanafunzi wengi wa shule za sekondari kukatisha masomo yao, ikiwamo wazazi wao kushindwa kulipia karo za shule kutokana na changamoto mbalimbali zikiwamo za umasikini” alisema.
Rais Kikwete alisema kufutwa kwa ada hiyo utekelezaji wake upo mbioni ili kuhakikisha kila mtoto anapata elimu bure, hatua ambayo itasaidia kuinua kiwango cha elimu nchini.

No comments: