Sunday, September 1, 2013

NAWATAKIENI JUMAPILI HII YA 22 YA MWAKA C IWE NJEMA !!

Mdada katoka kanisani hapa
 
Sala ya leo kwa ajili ya kuwaombea watu wote:
Salamu, Maria, umejaa neema, Bwana yu nawe,
umebarikiwa kuliko wanawake wote, na Yesu,
mzao wa tumbo lako amebarikiwa.
Maria mtakatifu, Mama wa Mungu,
utuombee sisi wakosefu, sasa na saa ya kufa kwetu.
Amina.
NA TUSISAHAU KUWAOMBEA JT. YUSTO, INGRID, JN GREGORI MKUU , SOFIA
JO ..ROSALIA, IRMGARD, AL.. ROMULO, ROSWITA...IJ ...MAGNUS, ALEX, JS YIDITH.
TUPO PAMOJA. AMINA

. 

11 comments:

Anonymous said...

Jumapili njema. Hivi huko kwenu bado mnafaidi jua? Naona umevalia mavazi ya summer na miwani ya jua kabisa. Mana hapa leo naona kabaridi tangu jana.

EDNA said...

Na wewe pia mdada, pia umependeza na nguo yako ya kiafrica

Rachel Siwa said...

Iwe njema kwako na familia pia..Umetokezea sana KADALA wa mimi.

ray njau said...

Jumapili njema kwa wadau wote wa kibarazani,

Yasinta Ngonyani said...

Usiye na jina hapo juu ahsante ..baridi haijaanza sijui mwenzangu upo wapi ila hapa kuna mabadiliko mara joto, mvua upepo nk....

Edna ..ulipotea nimekumiss ndugu yangu..
KACHIKI AHSANTE BÉ....
kaka wa mimi Ray!!Ahsante

Penina Simon said...

we Yasinta wewee, huyo mdada kwa kweli umemshonea kitenge kimempendeza!! unashona mwenyewe au kuna fundi huko huko wa kushona vitenge? nimependa aisee

ray njau said...

{kaka wa mimi Ray!!Ahsante}
Asante kwa kusema asante na mimi nasema asante sana da'Yasinta kwa kujali mchango wangu mdogo.Nakutakia mwanzo mwema wa wiki mpya.

Yasinta Ngonyani said...

Dada P! Hapa sijashonesha huku hii nilipata zawadi..Zinapatika dar..

Ray kaka wa mimi Mwanzo wangu wa juma umeanza vema namshukuru Mwenyezi Mungu.

ray njau said...

Dada wa mimi Yasinta uwe na mwisho juma wenye meme mengi kifamilia!

Mija Shija Sayi said...

Jamani dada mkuu unazidi kuwa msichana dadangu..

Umependezaje sasa..!!!

Yasinta Ngonyani said...

Kaka Ray! Ahsante nawe pia iwe hivyo!

Mija! umenichekesha kuwa mchichana? na wewe mwenyewe utasemaje sasa? Ahsante kwa kuona nimependeza:-)