Thursday, January 24, 2013

LEO:- TUSISAHAU VITENDAWILI VYETU/ JE UNAVIKUMBUKA HIVI?

1. Chini chakula, juu chakula, katikati kuni. Nini hicho
2.  Nimefika ugenini, ameniamkia mtoto. Mtoto huyu ni nani?
3.  Mtu anabadilika badilika
4.  Watoto wawili wanapigana kila wakati. Watoto gani hao?
5.  Ndege wangu ametagia kwenye miiba. Ndege gani huyyo?
6.  Shamba langu nimelima kubwa, nimepanda mbegu zangu tatu: Mbegu hizo ni nini?
7.  Mgeni yupo ndani nyumbani, hasemi, mimi simwogopi
8.  Nje kukavu, ndani maji. Nini hicho?
9.  Nyumba yangu ina nguzo mbili, kama zinaanguka siwezi kuzisimamisha.
10. Nimekata tete, nimevuka mto mkubwa. Tete hili ni nini?
11. Natoka kwa mama, naenda kufa.
12. Ugonjwa wa watu wote ni nini?
NAWATAKIENI KILA LA KHERI KWA KILA JAMBO...!!!!!!!

12 comments:

o'Wambura Ng'wanambiti! said...

UUuuuuwiii....hapo ntapata moja tu! Nambari 5 tu...ambalo ni NANASI

mengine yote mwalimu nipe yai tu bana!

Yasinta Ngonyani said...

mmmhhh! jaribu tena kaka Wambura maana hilo jibu si lenyewe...

Anonymous said...

1. Muhogo.

By Salumu

Yasinta Ngonyani said...

Makofi kwa kaka Salumu wa wa wa..umapata ....

o'Wambura Ng'wanambiti! said...

ayyaaaaaaa! NAFWAA

ray njau said...

Hakika ya kale ni dhahabu!
Asante sana Da Yasii.

Interestedtips said...

5. Nanasi
8. Yai
12. Njaa

Interestedtips said...

3. Kinyonga
hehehehe

Yasinta Ngonyani said...

naona wengi mmejaribu mnastaili zawadi kwa kweli ...au naona nitoa majibu yake..Ester umepata ya 12 na 3 makofi wa wa waaaaaa... hivi ni vitendawili vya kingoni kwa taarifa yenu na majibu yake ni:-
1. Muhogo
2. Miba ya nyasi(luhano)
3. Kinyonga
4. Miguu
5. Ulimi
6. Jua na mwezi
7. Kunguni
8. Tikitimaji
9. Matiti
10. Utandu wa buibui
11. Jani
12. Njaa

Interestedtips said...

Asante sana kwa majibu dada maana vilikuwa vigumuuuuuuuu

Vansh Chavda said...

Jibu hiyo kitendawili
1.hachelewi wala hakosei safari zake

Anonymous said...

1 muhogo