Wednesday, December 21, 2011

MVUA KUB WA YASABABISHA MAFURIKO JIJINI DAR ES SALAAM TANZANIA!!

Hapa ni baadhi ya wakazi wa spenco Vingunguti wakiwa wamekusanyika kusubiri boti iwaokoe.
Picha toka kwa michuzi-

6 comments:

Goodman Manyanya Phiri said...

Ndiyo hivyo, tena, maisha yetu duniani!!!


Aisee Poleni sanaaa!

ray njau said...

Kwa ujumla hali ni tete na vifo kadhaa vimeripotiwa na uharibifu mkubwa wa miundo mbinu ya usafirishaji.Athari kubwa ni ukanda wa mto msimbazi kuanzia pwani ya bahari ya hindi kuelekea Jangwani-Magomeni,Kigogo,Tabata-Segerea na Kinyerezi.Kwenye uwanja wa Kaunda eneo la Jangwani ukuta umevunjika na maji yapo usawa wa magoli.
Mamlaka ya hali hewa wanasema hizi ni mvua za msimu na ndani yake ni siku tatu zenye mvua nzito [Desemba 20-22,2011] na baadae hali itakuwa shwari.Lakini mvua hizi zimezusha maswali mengi na kuacha majibu machache.

issack che jiah said...

Tuwape pole sana ndugu zetu waliokumbwa na maafa haya,ila jamani tuache kungangania kaa mabondeni napale tunapopewa viwanja tusiuze ,napia serikali iwe na mikakati ya muda mrefu sio leo tukiona watu wanafanya kitu nje ya sheria viongozi munaanza kupingana kwani leo nimemsikiliza mkuu wa mkoa na mbunge wa kinondoni jinsi inavyoonyesha mamlaka yanavyoshindwa kutoa maamuzi maana kila mtu akiulizwa kibali anasema mimi nimepewa kibali na fulani nahuyo nae anasema vile hii si njema matokeo yake serikali inapata lawama kwaajili ya uroho na uchu rushwa inatawala
ni hayo
che jiah

Mija Shija Sayi said...

Mungu awatie nguvu watu wake.

Yasinta Ngonyani said...

Najiuliza je? kama tusingekuwa na ujenzi holela, na pia wale waliopewa majukumu ya ujenzi Je? tungekuwa janga hili la mafuriko kubwa hivi? Naona kama mtu aliyepewa majukumu kama angetenda kama ipasavyo basi tungekuwa na uokoaji wa urahisi zaidi.Ila nachoweza kusema pole sana waTanzania wenzangu. Mwenyezi Mungu na atupe ujuzi ,mawazo katika jambo hili.
Mungu ibariki Tanzania...Halafu nimesikia sehemu ni kwamba haijawahi kutokea mafuriko haya kwa miaka 50 iliyopita nikajiwa na wazo kichwani ni juzi tu tumetimiza miaka hamsini ya uhuru je? huu ni..... aaahh hapana. Nikaona niache...na nimeacha

cytotec said...

obat cytotec i think your blog very informative obat penggugur thanks for sharing obat telat bulan