Friday, August 14, 2009

UJUMBE WA LEO

Tabasamu la kawaida lina maana nyingi.
Hasa siku ambayo unajisikia vibaya,
Mimi nadhani wengi wanajisikia hivi,
Ndiyo, wote wazee na vijana.

Maneno machache yanaweza kuleta miujiza ,
Hasa katika muda mgumu,
Haya poteza na maneno ya upendo,
Unajua maisha yetu hayarudiwi,
Inabidi tufanye vizuri, kwa kila zuri.

5 comments:

Simon Kitururu said...

Amen!

Fadhy Mtanga said...

Hayo maneno ni matamu,
Ambayo huleta wazimu,
Tuseme hata nayo hamu,
Ya kutaka kutabasamu.

Nakupa nyingi salamu.

Nicky Mwangoka said...

Ni tafakari nzuri sana. Ulikuwa umeketi chini ya mti ulivyokuwa unafikiria hili nini?

Ramson said...

NA MIE NAKUPA NYINGI SALAAM......

Yasinta Ngonyani said...

Simon:-)
Fadhy! salamu zimepokelewa kwa mikono miwili.

Nicky! Ni kweli nilikaa chini mwembe....LOL.

Ramson! kwanza karibu sana hapa kibarazani kwangu na pia salamu zimepokelewa. Karibuni sana na sana..