Saturday, August 8, 2009

TUWE TUNAANGALIA TUKAAPO CHOONI INAWEZEKANA KUKAWA NA MGENI KAMA HUYU



Habari ndio hiyo ndugu zanguni.Haya nawatakienikila ka kheri wote wiki end njema. Kaazi kwelikweli!!!!

13 comments:

Nicky Mwangoka said...

Nimeogopa maana siwapendi hata kidogo maana walimwua bibi yangu, ila muhimu ni usafi Yasinta. Mdudu kama huyo hawezi kujihifadhi sehemu safi, huwa wanaenda sehemu chafu na kujificha.

Mzee wa Changamoto said...

Lahaulaaaaaaaaa!!! Ninawaogopa na kuwachukia hawa. Kwa kweli ni ama zao ama zangu. Kwa hiyo hapa ntakuwa naangalia mara kadhaa maana nimeogopa zaidi.
Lol

Albert Kissima said...

Da! De! Di! Do! Daaaa!

Kazi Kweikwei!

Fadhy Mtanga said...

Hakuna anaewaogopa wadudu hao kama mimi. Halafu nawachukia hadi huwa nakufuru kujiuliza kwanini wadudu kama hao waliumbwa.!

Anonymous said...

MIMI HUWA NAWAOGOPA SAAANA NA KUWACHUKIA LKN HAPA SWEDEN WANAUZWA KAMA PETS NA UNAKUTA MTOTO ANALALA NAE HADI KITANDANI JAMANI.KUNA NYUMBA 1 YA RAFIKI YANGU WA KISWEDISH MTOTO WAKE ANAYE NYOKA NA KENGE BASI NIKIENDA HAPO SIWEKI MIGUU CHINI NA NIKIONA ANAVYOMBUSU NASIKIA KUTAPIKA.

Faith S Hilary said...

Man who is not scared of a snake??? Na baada ya kuona hii picha, usiku akaingia bonge la buibui (spider), sorry I killed it. (not me ila I wanted it to be killed lol)

mzee wa matukiodaima habari bila uoga said...

Tukirejea katika Biblia inasema wazi kuwa Mungu aliomba bingu na vitu vyote vinavyoonekana na visivyo onekana hivyo kama naweza kusema vyote kwake Mungu vinautukufu japo kwetu binadamu tumekuwa waoga sana na kuogopa uombaji wa Mungu

Kama mchangiaji mmoja hapo juu alivyoeleza jinsi ambavyo Sweden wanavyopenda kufuga nyoka ama vile China hivyo tukiwapenda na kuwalinda bila shaka hawatatufanya vibaya

japo hawa ni hatari zaidi kwani kuzoeleka kwake ni vigumu ila Mungu ndiye muweza wa mambo yote .

Bennet said...

Huyu kiumbe ni hatari sana, nakumbuka siku moja tukiwa porini aliingia kwenye hema kuna jamaa anawajulia alimtoa kwa kumshika tu nilishangaa

Koero Mkundi said...

DUH!!!!!!!!!!!!!

chib said...

Kuna baba huko nchi za Asia alipata kadharuba kidogo kutoka kwa chatu mdogo aliyejificha katika choo ka ahuyu bw mkubwa. Chatu alijaribu kung'ata kitu fulani pengine akizani ni panya. Ila jamaa hakudhurika sana zaidi ya michubuko kidogo. Ni kweli kukagua ni muhimu

John Mwaipopo said...

ingawaje nishatwangwa mara mbili na nyoka maishani mwangu lakini hapana sipendi. ila hofu yenu na yangu vinaweza kuwa tofauti, pengine mimi siogopi kama mnavyoogopa nyie.

John Mwaipopo said...

ingawaje nishatwangwa mara mbili na nyoka maishani mwangu lakini hapana sipendi. ila hofu yenu na yangu vinaweza kuwa tofauti, pengine mimi siogopi kama mnavyoogopa nyie.

Yasinta Ngonyani said...

Nipo nanyi mi sipendi mdudu yoyote yule. Nimekumbuka kijana wangu aliweza kukua wiki moja bila kwenda haja kwa vile kulikuwa na mende. anawaogopa sana sio mchezo. Ila nyoka kazi kwelikweli bado sijawaelewa wtu wanaofuga nyoka ndani ya nyumba.