Monday, August 17, 2009

KUMBUKUMBU YA MAMA YETU

Mama Alana Magnus Ngonyani astarehe kwa amani.
Imepita miaka mitano leo tangu mama yetu mpendwa Alana Ngonyani aitwe na Mwenyezi Mungu kwenye makao ya milele, Agosti 17,2004. Mama Alana ameaga dunia akiwa na miaka 52.

Kutokana na pengo kubwa ulilotuachia na lisilozibika sisi watoto wako, mume wako, wajukuu wako, wakamwana na mkwe pia ndugu, marafiki na jamaa bado tupo nawe kwa njia ya sala na maombi. Kwa kuwa tunaamini kuwa Mwenyezi Mungu mwenye huruma amekupokea katika makao yake huko Mbinguni.

Kwa niaba ya familia ya marehemu tunawashukuru wote mliotusaidia na kujiunga nasi kwa hali na mali katika kuokoa uhai wa marehemu.

Aidha, tunawashukuru kwa sala katika kumsindikiza kwenye shamba la Mungu(pale Mkurumo) Mungu awarudishie mara mia wote mliojitolea kutusaidia.
Ee Mwenyezi Mungu umpokee mama yetu katika ufalme wako huko Mbinguni, Astarehe kwa Amani. Amina

15 comments:

Mzee wa Changamoto said...

N a apumzike kwa amani baada ya kazi ngumu ya malezi kwenu nyote.
Aliko, ajue kuwa kazi yake sasa yawa faida kwa wengi ulimwenguni.
Pumzika Mama

kamala Lutatinisibwa Lutabasibwa said...

ati apumzike kwenye makzi ya milele? kwani yale mengine yalikuwa temporary? mpaka lini tutajua kuwa hakuna kufa bali kuancha mwili tu?

PASSION4FASHION.TZ said...

Ee mungu, mpe raha ya milele na apumzike kwa amani, amina.

Koero Mkundi said...

Mama upumzike kwa amani, matunda yako uliyoyaacha duniani tunayaona...
tunajivunia dada yetu Yasinta Ngonyani

Nicky Mwangoka said...

Jamani, inaumiza unapomfikiria uliyempenda kwa dhati hauko nae tena kimwili. Yasinta ,mama alikupa malezi mazuri sana na hadi sasa unafurahia maisha.Haya na mengine mema mengi aliyofanya mama yamstahilie raha ya milele. Awe mwombezi wetu. Apumzike kwa amani.Amina.

Bennet said...

Pengo aliloliacha halitazibika kamwe, mlimpenda na kumwitaji sana lakini muumba alimuhiitaji zaidi akamwita

Anonymous said...

Hello Ngonyani,
Pole sana kwa kuondokewa na Mama!
Nani kama mama? Kweli Furaha hupungua mama akitangulia.
Lakini kwa wakristu, na waamini wa dini nyingi tunambua mama hajafa kabisa isipokuwa uzima wake umegeuzwa tu na kufanana na wa Muumba wetu. Kumbe bado Mama Kiroho anakupata kila mahitaji ukimuomba na kumuombea. Nitatolea misaa kwa ajili yake na marehemu wote.
Pili, nitoe masikitiko yangu.Nimeshangaa sana wewe umevaa vizuri alafu Mama ndo unaweka picha yake hiyo..Ni kukosa Heshima impasayo mzazi huyo. Bora usingetuwekea picha kwa maoni yangu. Maana mama wa Dada NGONYANI ni heshima yetu na ni mama yetu pia.Kama huna hata passport size..ondoa picha hiyo..haina hadhi ya mama..ni kumchezea mama na kumfananisha na vijimiss vya Songea. Mpe hadhi hata kama hakuna picha wake ua waridi, Ndo maana maana hata Bikira Maria alipopalizwa aliacha maua waridi kwenye kaburi lake, na yule mtume Yohana ambaye hakuwepo aliporudi alikuta maua. Mpe mama heshima yake. Ni kero ndogo tu ambayo mimi nimeona wengine sijui wanasemaje.

Kila mtu na jicho lake..X2

Mungu umpe Mama yetu huyu raha ya Milele na mwanga wa milele umuangazie. Upumzike kwenye amani na ufalme wako mbinguni Amina.

Msukuma

Masangu Matondo Nzuzullima said...

Uchungu wako Yasinta unasikika vyema. Ni sawa. Yeye ametangulia na kama unaamini, basi siku moja utakutana naye tena. Alifanya kazi nzuri sana ya malezi na leo hii jamii yote tunafaidi. Mama anaishi kupitia kwako na hata kwa sisi ambao hatukumfahamu, tunamfahamu yeye alikuwa mama wa aina gani kupitia kwako. Apumzike kwa amani!

chib said...

Pole sana

Anonymous said...

Pole sana Dada.Mwenyenzi Mungu ampe Mama pumziko la amani.AMEN

Unknown said...

Nami ningependa kuungana na wadau waliotangulia kumtakia mama pumziko la amani, sisi tulimpenda, lakini mungu alimpenda zaidi....

Simon Kitururu said...

Pole sana!

Yasinta Ngonyani said...

Asanteni sana wote maana nilikuwa sina nguvu kabisa. Kwa kusoma maoni yenu nimejikuta nimepata nguvu mpya na nimefarijika sana: Mbarikiwe sana na yeye muumba wetu.Ahsanteni sana.

Anonymous said...

[url=http://firgonbares.net/][img]http://firgonbares.net/img-add/euro2.jpg[/img][/url]
[b]macromedia flash5 software, [url=http://firgonbares.net/]store manager software[/url]
[url=http://firgonbares.net/][/url] kaspersky virus microsoft office 2003 key generator
academic licensed software [url=http://firgonbares.net/]academic priced software[/url] selling a software
[url=http://firgonbares.net/]biggest discount software[/url] oem software package
[url=http://firgonbares.net/]cheap computer software[/url] Poser 7 Mac Poser
autocad lisp [url=http://firgonbares.net/]use oem software[/b]

Anonymous said...

[url=http://bariossetos.net/][img]http://vonmertoes.net/img-add/euro2.jpg[/img][/url]
[b]macromedia flash 5 software, [url=http://hopresovees.net/]i buy oem software[/url]
[url=http://bariossetos.net/][/url] discount software sales buy microsoft office 2003 software
student discount softwares [url=http://vonmertoes.net/]nero cd burner[/url] Toast 10 Titanium Pro
[url=http://bariossetos.net/]nero 9 nzb[/url] academic discounts software
[url=http://bariossetos.net/]free adobe software[/url] office software uk
writing queries in filemaker pro [url=http://hopresovees.net/]photoshop elements for mac 4[/b]