Friday, June 27, 2008

JUNI 27, 2008 CHAKULA


Ugali , maharage na chainizi . huu ulikuwa mlo wangu mwaka jana wakati nilipokuwa TZ Ninawashauri watu wote kula chakula hiki ni kitamu sana. Isipokuwa kama umezoea kula samaki na dagaa itakuwa ngumu kidogo.
Na; Yasinta Ngonyani

4 comments:

Unknown said...

Umenikumbusha mbali sana kwa kweli, Nilikuwa na bustani ya uhakika nyumbani kijijini kwa wazazi wangu basi nilikuwa nachuma hilo chenese cabbage, ugali na maharage yanaungwa halafu ni fresh, hapo napata huo mlo baada ya kuchapa jembe la mkono kweli ugali ulikuwa unakuwa mtamu jamani, acha hapa tunakula mboga imekaa miezi mitatu kwa jokofu.

Yasinta Ngonyani said...

Kamwene! Kaka Mbilinyi asante kwa maoni yako. Unajua ninajaribu kupanda mchicha,chenesi, figiri na mboga nyingine za majani si unajua kama vile Nyamuza(kibena) najaribu kidogo kibena

Anonymous said...

Mmm najisikia njaa!huu ugali kaweka nani?Nitapiga mtu ngumi hapa kwanini hamjaweka samaki.Mbona hakuna kambale,vitui,mandongo,mbasa,mbelele.ngorokoro,dagaa halafu ugali huo siyo wa muhogo.Jamani sitaki tabia yenu ya kunikaribisha ugali ambao hauna hata matembele wala mlenda...sitaki nimesema Mmm mtajuaje kama mimi mnyasa natania jamani hata sijakaribishwa naanza mikogo.Hakika ugali ni mlo adimu duniani na wasiokula wafanye hadidu rejea wawe na mawazo jadidi angalabu yakasaidia kutafuta ugali wa muhogo...
mwenga kunoga mmmh leta samaki

Anonymous said...

Hii ndio sababu hakuna samaki kwenye sahani kwa vile sio ugali wa muhogo.