Wednesday, June 18, 2008

Juni 18, 2008 SHAIRI (KWA NINI?)

Kwa nini vitu kama hivi vinazaliwa,
Yaani ambavyo havihitaji kuishi.

Kwa nini vitu kama hivi vinaota
ambavyo havitakiwi kuvunwa

Kwa nini mimi kila wakati nakuwa nimeshiba
wakati wengine wengi hawana chakula

Kwa nini zinatengenezwa silaha nyingi sana
kwa ajili ya kuua?

Kwa nini hatuwezi kufunzana
vipi kupokea shida za wengine

Kwa nini hatuwezi kujifunza kuwa waangalifu
kwa yetu wetu ulimwengu na yetu paradiso

Kuna maswali mengi,
ambayo hayana majibu, duniani hapa na yenye ahadi za uongo


Na; Yasinta Ngonyani

No comments: