Monday, June 16, 2008

Juni 15,2008 MAHITAJI/CHAKULA/ USAFIRI

Tumwombe mungu ili hali hii isiendelee; Yaani Bei ya chakula imepanda, bei ya mafuta imepanda pia. Usafiri umekuwa ghali eeh jamani mbano tutakufa sasa kwani hatutaweza kwenda hospitali. Na je? tutalalaje bila mafuta ya taa? Na je tutapikaje bila mkaa angalia pia ada za shule kweli tutaweza kusoma? Kama nakumbuka vizuri watu wa zamani walisema ukiishiwa sana usikose chumvi ndani ya nyumba lakini sasa hiyo chumvi itapatikanaje? Je? hizo bajeti haziwezi kurudiwa kupangwa tena kwani watu tunaumia.


Na; Yasinta Ngonyani

No comments: