Friday, June 13, 2008

Juni 13,2008 LIKIZO

Leo ni siku ile ambayo shule zote ulimwenguni zimefungwa. Ila sasa sikiliza, wanafunzi hapa wao wanalikizo ndefu sana wiki kumi. Yaani mpaka mwezi wa nane tarehe 19. Sababu kubwa ni kwamba hakuna kipindi kingine watu wanaweza kufurahia joto, kuonana, kula na kunywa na marafiki. Ooh nilitaka kusahau kitu muhimu sana kuogelea kwani si mnajua tena, baridi yaani kuanzia mwezi wa tisa mpka wa nne(tano) ni baridi tu nadhani nimeandika kuhusu Hali ya hewa kwa hiyo rudi nyuma na usome tena kama umesahau. Yaani hapa watu wanaona jua (joto) miezi mitano(sita) kama hivi. Sasa labda watu wataonekana nje, kwani hatuonani kabisa wakati wa baridi kila mtu ndani tu. Maisha ya Ughaibuni ndugu zanguni mmmmmmh ..........tuache hivyo hivyo kwani waswahili wanasema ukikuta wanyeji wanatembea uchi basi nawe tembea.

Na; Yasinta Ngonyani

1 comment:

Anonymous said...

mimi nina penda kufunga shule!