Monday, August 15, 2016

TUANZE WIKI HII/JUMATATU HII NA HILI NENO KUSAMEHE:- KUSAMEHE NI MTIHANI/JITAHIDI USHINDE!

Katika tembea tembea nimekutana na hii makala kuhusu kusamehe....nikaona Elimu hii nisiwanyima ndugu zanguni..karibu muunganie nami.... 


Katika maisha hakuna jambo gumu kama kusamehe na hakuna kitu chenye faida kama kusamehe. Kuna watu katika maisha wapo ili tuumie na TUJIFUNZE. Wengine wapo ili tukisha umia wao watuumize zaidi ili tukose imani kwa wengine!
Lakini katika wote, wapo ambao kazi yao ni kutufariji, wao Inawezekana walipitia magumu kama yetu hivyo wana fahamu njia ya kutokea lakini kwa sababu tuliumizwa zaidi hatutaki kuwaamini hata wao. Ukisamehe unaweza kuamini upya!
Ni kweli katika maisha bila watu kama hao hatuwezi kuitwa "imara". Umewahi KUJIULIZA kwanini mtu anaitwa MVUMILIVU?? Kipimo chake ni kipi?? Uwezo wa kusamehe na kusonga mbele bila malalamiko ndiyo UVUMILIVU HALISI.
HAUNA jambo gumu kama kusamehe maumivu ambayo yanajirudia kichwani, yana choma moyo kama panga kali...... Vuta picha mtu anakuumiza alafu vilevile anataka akumalize kabisa! Alafu baada ya kuumbuka anaomba msamaha!
Vuta picha umemfumania mkeo au mume wako alafu una ambiwa samehe! Vuta picha mtu kamuua mzazi wako au ndugu yako kisha una ambiwa samehe! Moyo unauma, akili inakataa, mwili unawaka hasira lakini bado una ambiwa samehe, jikaze tu!
Wengine walikusababisha uishi maisha ambayo unaishi kwa sasa, unatamani hata wafe! Lakini una ambiwa samehe! Msamaha ni nini hasa?? Unalia ukijipiga kifua, msamaha ni nini?? Machozi ya uchungu yanakutoka kujaribu kuosha hasira yako lakini moyo unakataa!
Utaimba nyimbo zote za kujifariji lakini moyo unasema HAPANA NIMEUMIZWA SANA. Unashindwa kula na kulala vizuri kwa sababu umeumia! Mbaya zaidi hisia zikiumia ni hatari kuliko Simba aliye katwa mguu! Na wengi wana umizwa sana kwa sababu ya kitu kimoja tu IMANI.
Wengi leo wame umizwa sana na Mama mkwe, shangazi, wazazi, ndugu, marafiki, wapenzi, majirani na kadhalika! Lakini tiba ni moja tu, KUSAMEHE. Kutokusamehe ni sawa na kumsaidia shetani kufanya kazi maana mawazo yako yatakuwa sawa na shetani anavyo waza (uharibifu).
Kusamehe ni tiba ya presha, ni tiba ya kichwa na moyo. Kusamehe ni dawa ya maisha na pia ni baraka kwako! KUSAMEHE kunamfanya MUNGU akuamini ili upande daraja la imani la kiwango kingine cha juu zaidi.
Nakumbuka katika maisha yangu, nimewahi KUUMIZWA mara nyingi tu katika mambo tofauti tofauti, lakini mara zote napata somo jipya. Pamoja na kujifunza sana lakini kuna muda ilinibidi NISAMEHE KWA MACHOZI, yaani nasamehe nikiwa natokwa machozi kwa lengo la kuuponya moyo wangu!
Ni kweli umeumia lakini Samehe sasa, samehe leo, samehe kesho, samehe siku zote! Binadamu wana umiza sana sana sana tena sana lakini jivike moyo mkuu, samehe ili maombi yako yakubaliwe na MUNGU. Kumbuka msamaha ni tiba, ni amani ni upendo ni faida.
NB: Kwa yeyote aliye wahi kuniumiza kwa namna yoyote ile NIMEMSAMEHE, kwa yeyote yule anaye ona nimemuudhi na anisamehe, kwa yeyote yule ambaye huwa anahisi sijamsamehe na afahamu sasa kwamba NIMEMSAMEHE asitazame ukubwa wa kosa au mazingira ya ugomvi, atazame utumishi na huruma ya MUNGU ndani yangu, amen.
CHANZO: Na Charles Francis M,

No comments: