Thursday, August 4, 2016

MAISHA NA MAFANIKIO:- JIKUBALI

 MFANYABIASHARA WA KUUZA MBOGA ZA MAJANI AKIKOKOTA BAISKELI 

Maisha ya watu wengi sana yanashindwa kufanikiwa kwa sababu watu hawajikubali. Ngoja nikuambie kitu leo:- Kila mwanadamu aliyeumbwa hapa duniani, ameubwa na kitu tofauti na mtu mwingine. Hii ina maana kwamba kila mwanadamu ana kitu tofauti kikubwa ambacho anaweza kukifanya hapa duniani kuliko mtu mwingine. Japo sikuambii wewe ni bora kuliko watu wengine, lakini ninachokuambia wewe una kitu bora zaidi cha kufanya katika  maisha yako kuliko watu wengine.
Tatizo kubwa wanalolifanya  watu wengi wasiweze kufanya vile ambavyo wanataka ni kutokujikubali. JIKUBALI. Tunaweza tukazaliwa tumbo moja, tukasoma darasa moja, lakini wote tukawa na kitu ambacho kitatutofautisha. Kinachokufanya uendelee kuwa hivyo ulivyo ni kwa sababu tu haujikubali na haujiamini kuwa wewe ni mtu tofauti.
Ngoja nikumnie kitu kingine  tena,  wewe ni mtu tofauti sana, na unaweza kufanya vitu vikubwa sana kwenye hii dunia. Lakini kitu pekee unapaswa kukifanya kuanzia  leo ni KUJIKUBALI. Usikubali mtu akukatishe tamaa, JIKUBALI, usikubali mtu akuambie hauwezi...JIKUBALI, asikuambie mtu hauwezi kufanya hicho unachofanya . ANZA KUJIKUBALI unapojikubali mambo mengine yanakuwa rahisi. Hata kama leo unahaingaika na magonjwa kiasi gani usikubali kuambiwa nawengine JIKUBALI WEWE, ukijikubali utapata nafuu.
Kulikuwa na dada mmoja mzuri sana, lakini kasoro yake ilikuwa moja tu alikuwa na matege. Alichokifanya dada huyu ni kuvaa nguo fupi ili watu waone matege yake....ALIJIKUBALI na watu wakamkubali.
Tatizo kubwa tulilokuwa nalo sisi au watu wengi ni kutoJIKUBALI. Kujificha ule uhalisia wao, kujificha ule mwonekano wao halisi wa wao na hii inawafanya maisha yai kutokubalika kabisa. Ushauri wangu JIKUBALI ULIVYO halafu kila siku songa mbele. ukijikubali na wengine watajikubali. Ndugu yangu jikubali kwa hali yoyote uliyo nayo leo ili ikufanye usonge mbele.

2 comments:

ray njau said...

Ni hakika na kweli!!

Yasinta Ngonyani said...

Kaka Ray...ahsante kwa kupita hapa na kuacha lako la mu-mutima...