Monday, April 4, 2016

WIKI HII IMEANZA VIZURI KWANGU:- NIMETUMIWA ZAWADI ZA VYAKULA NIVIPENDAVYO:-)

 Kwanza Samaki kutoka  huko Mwanza ...jina nimesahau
 Halafu kumbikumbi
Na mwisho  ni BOGA  kwa kweli nimefurahi sana sana maana ni haswa baadhi ya vyakula nivipendavyo ambavyo naweza nikala kila siku bila kuchoka:-) Je? Wewe unayesoma/angalia hapa una chakula pia ukipendacho sanaaa? JUMATATU NJEMA KWA WOTE!!

4 comments:

Ndugu Nkwazi N Mhango said...

Njoo Kanada utakula hao samaki na maboga hadi uvimbiwe. Tusichokuwa nacho hapa ni hao kumbikumbi tu. Nao nitafanya utafiti nione kama wapo au hawapo.
Endelea kufaidi ila ule kwa kiasi dada yangu.

Yasinta Ngonyani said...

Hahahaaaa :-) Kaka Mhango nimecheka hadi nahisi....machozi yanatoka . Eti Nije Kanada kula mabogo na Samaki na pia upo katika mkakati wa kutafiti kumbikumbi...Kaaazi kweli kweli ama kweli jumatatu hii imekuwa njema:-)

Salehe Msanda said...

Hao samaki wanaitwa sato, watani wako wapogoro wanaita Perege
Kila la kheri

















Yasinta Ngonyani said...

Kaka Salehe! Ahsante sana Hayo majina yote yalikuwa kichwani mwangu ila sikujua kama ni samaki mmoja:-)