Friday, April 8, 2016

PALE TUNAPOYACHUKULIA MAISHA KIRAHISIRAHISI

Kama utayachukulia maisha kuwa ni dharura ni wazi utakuwa unakasirishwa hata na vitu vidogovidogo. Unapohisi kwamba, unaelekea kwenye kukasirika, unapaswa kujiambia au kujikumbusha kwamba, maisha siyo dharura. Kuyachukulia maisha kuwa siyo dharura ni pamoja na kujua kwamba, migogoro ya kimaisha ni jambo la kawaida na haiwezi kuepukika. Kujua kwamba, kukasirika hata siku moja hakuwezi kutatua matatizo yetu, badala yake hutuingiza kwenye matatizo makubwa zaidi kimwili na kiakili.
CHANZO:- KITABU CHA MAISHA NA MAFANIKIO

2 comments:

Nicky Mwangoka said...

Ni kweli kabisa dada. Ushauri mzuri

Yasinta Ngonyani said...

Ahsante kaka Nicky...PAMOJA DAIMA!