Thursday, April 21, 2016

PICHA YA WIKI:- UNAKUMBUKA HII MIAKA ILEEEE

Nina uhakika hii itarudi tu. Maana yote ya kale yanarudi sasa... yaani hii ilikuwa kila aliyekuwa na pasi alikuwa nayo na kama huna unaenda kwa jirani/rafiki na kunyoosha hivyo...Je? ww uliwahi kunyoosha shati lako hivyo?

6 comments:

Anonymous said...

duh nimecheka sana mpaka ofisini wakawa wananiuliza...

looh tumetoka mbali sana.

Dottie

Yasinta Ngonyani said...

Dottie! Kwanza karibu sana kibarani hapa. Pia ahsante sana kwa kuacha yako ya moyoni. Nimefurahi umefurahia hii na kukumbuka enzi zileee...

Penina Simon said...

Jana na juzi umeme kwangu hamna,
yaani nimeikumbukaje hiyo pasi jamani!!!!, mbona nitainunua tu tena niliziona Buguruni halafu zina shape nzuri sana siku hizi

Yasinta Ngonyani said...

Dada P... Ulichosema ni kweli kabisa, sio kutegemea umeme tu inabidi kujiandaa. Kama majiko...inabidi Uwe na mkaa nyumbani au gesi. Hata mswaki inabidi Uwe na ile miswaki yetu ya kienyeji.:-)

sophie said...

Yasinta asante saana maana sina mbavu! watoto wangu wameiangalia hiyo pasi hawaamini pasi inafanana hivyo.asante kwa picha hii.

Yasinta Ngonyani said...

Sophie.. Mwenyewe hapa nimepata maswali kiasi kwamba nimeshindwa kujibu...Itabidi ukanunue pasi Aina hiyo ili wajaribu kutumia ila inabidi Uwe karibu ....:-)