Thursday, April 28, 2016

JINSI YA KUPIKA MABUMUNDA/MIKATE YA NDIZI!

Nimekaa hapa huku nikuota/kumbuka jinsi tulivyokuwa watoto na tulivyoanza mapishi kwa mfano hiki chakula  cha makte wa ndizi/mabumunda  kule Lundo tulikuwa tukipika sana na hata kujipatia tusenti twa kununua pipi:-) Haya karibu  labda nawe kuna chakula ambacho ulianza kupika ulipokuwa mtoto..... NI HIVI:-

MFANO WA MABUMUNDA
MABUNDA ni aina ya chakula cha asili cha Afrika ambacho ni rahisi kukiandaa. Pia kinajulikana kama MKATE WA NDIZI Kwa lugha nyingine.Ni chakula kilicho katika mfumo wa mkate ila hiki upikwa na ndizi na unga wa mahindi.

MAHITAJI
> Ndizi mbivu zilizoiva vizuri au hata kukaribia kurojeka.

> Unga wa mahindi ila nzuri zaidi kama utatumia unga wa dona.

> Jani la mgomba.

JINSI YA KUPIKA

Menya ndizi zako na uziweke katika kinu kidogo kisha ziponde hadi zilainike na kuwa uji uji.Baada ya hapo,zitoe ktk kinu na weka katika bakuli kisha changanya unga wa mahindi hadi mchanganyiko wako ukolee.

Osha jani la mgomba vizuri na ulipitishe ndani ya moto ili lilainike.Kisha kata jani la mgomba vipande na chukua ule mchanganyiko wako wa unga na ndizi na uuweke katika jani la mgomba vizuri kisha ulisokote.

Weka katika sufuria au chungu na ubandike jikoni katika moto mkubwa kiasi.Funika na mfuniko wa chuma na juu paria moto kama unavyopika waki.

Subiri kwa dakika kumi au kumi na tano na ugeuze bumunda lako.Baada ya kuiva litakuwa gumu,hivyo tegua na ondoa mabaki ya majani ya mgomba na uache bumunda lako lipoe.

FAIDA ZAKE

=Ni chakula kinachodumu kwa muda mrefu bila kuharibika (kuchacha).

=Hakina madhara ya kemikali kama mikate ya viwandani.

Unaweza kula wakati wowote,waweza kunywa na chai au hata uji, pia usisahau juice AU tu maji

"Onyesha ufahari kwa kula vyakula kwa kula vyakula vyenye asili ya mtanzania"

Maswali na ushauri vinaruhusiwa.....TUPO PAMOJA!

No comments: