Monday, April 25, 2016

TUANZE JUMATATU HII KWA KUANGALIA WANYAMA KATIKA MBUGA TOFAUTI AFRIKA/TANZANIA

 Hapa ni Pundamilia hawa si wakali sana ni kama vile farasi tu ....
 Hawa wanaonekena wazuri na wapole lakini ukikutana nao hawana huruma maana  watakuona kitoweo ..SIMBA. Nilipokuwa nikiishi Madaba/matetereka kulitokea simba na wakawa wanasema ya kuwa tusiogombe ya kwamba simba hali watu. Mie sikuwaamini ....sijui nilikuwa mwoga mno???
 Tembo huwa wana hasira za haraka sana au sijui za ziada pia....
TWIGA WA MANYARA
Hakuna wanyama niwapendao kama TWIGA... wana mwendo wa maringo  na ukizingatia wana shingo ndefu pia miguu Yao mirefu. Je wewe una mnyama umpendae?

No comments: