Wednesday, March 25, 2015

UTANI KIDOGO- MLEVI NA MCHUNGAJI WAMEKUTANA!!

Ungana nami na utani huu nimeona si vizuri kupata elimu hii peke yangu ...nimetumiwa na msomaji wa Maisha na Mafanikio. KARIBU.....


MCHUNGAJI; "Unakunywa bia!?      
MLEVI; "Ndio.
MCHUNGAJI; "Kwa siku unakunywa bia ngapi!?
MLEVI; "Nakunywa bia tano!
MCHUNGAJI; "Bia moja bei gani!?
MLEVU; "2500/
MCHUNGAJI; "Ulianza lini kunywa bia!?
MLEVI; "Miaka 18 iliyopita!
MCHUNGAJI; "Kwa hiyo kwa siku unatumia zaidi ya 10,000??
MLEVI; "Ndio!
MCHUNGAJI; "Kama u gekuwa unatunza hiyo pesa 10,000 kwa siku leo hii si ungekuwa na Range Rover!?
MLEVI; "Samahani, naweza kukuuliza swali!?
MCHUNGAJI; "Uliza!
MLEVI; "Unakunywa bia!?
MCHUNGAJI; "Hapana!
MLEVI; "Nionyeshe Range Rover yako!
MCHUNGAJI; "Akakimbia.....

9 comments:

Anonymous said...

Safi sana! Hapa ujumbe ni usihukumu kabla ya kujihukumu. By Salumu.

mikidizo said...

KUNA HII HAPA YA MWALIMU WA KISWAHILI NA MWANAFUNZI

MWALIMU: Sadiki tunda sentensi yenye neno SUKARI

MWANAFUNZI: Chai yaleo nitamu sana

MWALIMU: Sadiki sasa likowapi neno SUKARI?

MWANAFUNZI: SUKARI ipo ndani ya chai

by mikidizo

Yasinta Ngonyani said...

Kaka Salumu hakika umenena na hili huwa linatokea kila siku ya Leo. ...tunakuwa haraka sana kuhukumu wengine.

Mikidizo! Kwanza kaeibu sana Maisha na Mafanikio. Ahsante kwa hii ama kweli nimecheka mno.

ray njau said...

Hahaha!

Yasinta Ngonyani said...

Si umeona eeehh kaka Ray!

Ndugu Nkwazi N Mhango said...

Watoto wawili watundu.
Mtoto Mtundu wa Kwanza: Unajua chini ni wapi?
Mtoto mtundu wa pili: Wewe unajua juu ni wapi?
Mtundu wa kwanza:Juu si juu tu.
Wa pili: Chini si chini tu.
Mtundu wa kwanza: Ukiwa juu unaona chini.
Wa pili: Ukiwa chini unaona juu.
Mtundu wa kwanza :Kumbe juu na chini ni sawa?
Wa pili: Kwani mimi nawe ni sawa?

Yasinta Ngonyani said...

hakika hakuna siku nimecheka kama leo kaka Mhango umenichekesha mno ,,,,

Ndugu Nkwazi N Mhango said...

Da Yasinta kicheko dawa. Cheka tu cheka sana tu. Nami nacheka na wakati mwingine naandima mambo ambayo hunichekesha.

Yasinta Ngonyani said...

Kaka Mhango naendelea kucheka nawe cheka sana sana:-)