Tuesday, July 9, 2013

MATUNDA NA BEI YAKE..KAAAZI KWELIKWELI......

Jana nikawa na hamu kweli ya papai nikaenda dukani kuangalia bei mamaaa weeewewee kama muonavyo hapa 22kr ni sawa na 5000Tsh na kapapai ndo kama ngumi yangu...nikaanza kukumbuka mapapai yangu Ruhuwiko kwangu..nikaondoka na sikununua papai. Maisha haya kaaaaazi kwelikweli..

8 comments:

Unknown said...

Mmh pole huku Mia 5 papai kibao

Justin Kasyome said...

kweli kbs, ugenini tunapata shida sana ya bei za vitu ambavyo nyumbani viko chini!pole kwa hilo ila ishi maisha yalivyo ili kuepuka ugonjwa uitwao "kiu ya kweli!"

ray njau said...

Mhhhhhhhh;nyumbani eeeeeeeeeh,nyumbani ni nyumbani japo hakuliwi!!!

Yasinta Ngonyani said...

Nancy! Ahsante aisee....na hongera

Kaka justin ! Umeona hiyo eeeh yaani hapa nipo hoi....
Kaka wa mimi Ray ....wewe acha tu..

Anonymous said...

Sasa hii ni fursa yako da Yasinta. Unaweza kuimport mapapai toka TZ na ukapata faida zaidi ya 500%. Ramadan Kareem to all. By Salumu.

Anonymous said...

Dada Yasinta nilikuwahi kukupa siri ya matunda nje, usilinganishe bei na kukumbuka ya shambani kwako mana ni ya bure, ukiwa na kiu ya tunda nunua tu kula ukimaliza ndio uanze kulinganisha bei na kukumbuka ya nyumbani! Ila pia licha ya bei hayana utamu kama wa ya nyumbani. Hongera kwa kuyatazama na kutonunua. Sasa huwa unapendelea matunda yapi ambayo bei yake ni nzuri kwa huko ulipo?

Mija Shija Sayi said...

Bahati nzuri ni kwamba kila sehemu matumizi huendana na mapato..

Yasinta Ngonyani said...

Haya kaka Salumu ni wazo nzuri ahsante.

Usiye na jina nimekupata.

Dada mkuu msaidizi ahsante.