Monday, July 15, 2013

KWA NINI WANAUME WANASHINDWA KULING'AMUA HILI?

Kuna wakati niliwahi kueleza juu ya wanaume kudhani kuwa kuwanunulia wake au wapenzi wao kila kitu kwa maana ya nyumba nzuri, magari ya kifahari na mavazi ya thamani, inatosha kupeleka ujumbe kwa mke au mpenzi wake kuwa anapendwa. Nilieleza kwa kirefu sana juu ya dhana hiyo jinsi isivyo sahihi na niliweka bayana kuwa, wanawake ni viumbe wanaohitaji kusikilizwa kuliko kitu kingine, bila shaka mlio wengi mnakumbuka makala hiyo.

Kwa asili wanaume wanapenda sana kuwasikia wake au wapenzi wao wakikiri kuwa wanawapenda na kufurahia tabia zao nzuri wema walio nao, vipaji walivyo navyo na sifa nyingine lukuki. Wanaume wanapopewa sifa za aina hii na wake au wapenzi wao hufurahia na kupata nguvu na kuona kwamba wana thamani kubwa mbele ya wake au wapenzi wao, kinyume na hivyo wanaume hukerwa na kutowajali wake zao.

Pamoja na kuoneshwa upendo lakini hata hivyo hiyo haitoshi kuwafanya wanaume wawapende na kuwajali wake au wapenzi wao. Kuna wakati mwanaume anakuwa na kazi nyingi sana na anatumia muda mwingi kwenye kujisomea au kuangalia Luninga, hata pale mke au mpenzi wake anaponyesha kwamba anahitaji kuwa naye kwa muda fulani. Kuna wakati pia mwanaume anajali zaidi kazi zake kuliko mambo mengine ambayo mkewe anayataka na kuyaona ya maana.

Naamini wengi mtakuwa ni mashahidi wa kauli hizi, “Yaani niache kazi zangu nikae kukusikiliza wewe na upuuzi wako, subiri nikipata muda tutaongea mambo hayo” kauli hizi ni sumu kali sana katika uhusiano, na huchangia kwa kiasi kikubwa ndoa na mahusiano ya wapenzi wengi kuporomoka.

Ni kweli kuwa kuna wakati mwanaume anaweza kuwa bize na shughuli zake,lakini pale mke au mpenzi wake anapohitaji ukaribu na yeye ni wajibu wake kuonesha kujali.
Kama mwanamke anahitaji kufanya jambo fulani ambalo inabidi mwanaume amsaidie, lakini inapotokea mwanaume kuonyesha kwamba hajali sana juu ya jambo hilo bila kujali kama yuko bize au hayuko bize, mwanamke huhisi kutothaminiwa na hiyo humuumiza sana kihisia. Lakini kama mwanaume ataonesha kujali hisia za mkewe na kumsikiliza kwa makini hata kama hatatoa ushirikiano hiyo tu inatosha kumridhisha mke au mpenzi kuhisi kuwa anapendwa na anasikilizwa.

Lakini utakuta wanaume wengi hawajali utashi wa kihisia wa wake zao na huamini kwamba wanawake wanachohitaji ni kupewa fedha au mali na kuhakikishiwa maisha ya kifahari basi.
Ukweli ni kwamba wanawake wanahitaji sana kusikilizwa hisia zao na kupewa nafasi pekee na mume au mpenzi wake pale anapohitaji nafasi hiyo ya kusikilizwa. Kumuonesha mwanamke kwamba hana thamani na hana nafasi ya kusikilizwa na badala yake kazi na kusoma, au kuangalia luninga kukaonekana ndio kuna thamani kuliko yeye ni kosa kubwa.

Ni jambo la msingi sana kwa wanaume kulifahamu hili kwa ustawi wa ndoa au mahusiano yao na wake au wapenzi wao, kwani wanawake wanahitaji nafasi kutoka kwa wanaume au wapenzi wao zaidi ya kitu kingine, maana hayo mengine yatakuja kujazia tu

6 comments:

Unknown said...

Ni kweli kabisa Da yasinta ila kwa kipindi hiki huwezi kumpata mwanaume wa hivyo wanaume wa sasa ni majanga matupu wanataka wasikilizwe wao tu.

Yasinta Ngonyani said...

Nancy! Nakubaliana nawe lakini labda niseme kwamba sio wote ..au tuchukue ule msemo kuwa samaki akioza mmoja ....na hapa ni kwamba ni baadhi wapo hivyo na hii yote inatokana na malezi aliyopata....

Justin Kasyome said...

asante kwa elimu hii maana hata sisi ambao hatujaingi katika ndoa, tunapata ufahamu!walah, hap nimepata shule na sitafanaya kosa hilo kamwe!

Amina said...

Namshuru mungu mume aliyenipa ananisikiliza sana naomba tu asije akabadilika maana hawakawii kubadilika hawa

Unknown said...

Nampenda na kumthami sana mke wangu Esther Avelline.

Nipo nae pichani,

ray njau said...

Ni Nini Kinachofanya Ndoa Ifanikiwe?
=================================
Wenzi wengi wa ndoa wana kumbukumbu nzuri sana za uchumba wao. Walifurahi sana kumfahamu yule ambaye angekuwa mwenzi wao wa ndoa! Kadiri walivyotumia wakati pamoja, ndivyo walivyokuwa na uhusiano wa karibu zaidi. Lakini, iwe walioana baada ya kuchumbiana au walifunga ndoa iliyopangwa, mwishowe wakiwa mume na mke, ilikuwa muhimu wafanye marekebisho fulani. Mume mmoja anasema hivi: “Tatizo kubwa tulilokuwa nalo mwanzoni mwa ndoa yetu lilikuwa kutambua kwamba hatukuwa tena waseja. Kwa muda fulani ilikuwa vigumu kushughulika na marafiki wetu na watu wa familia kwa usawaziko.” Mume mwingine, ambaye amekaa katika ndoa kwa miaka 30 sasa, alitambua mapema katika ndoa yake kwamba ili kuwa mwenye usawaziko, alihitaji kujifunza “kukumbuka kwamba ana mwenzi.” Kabla ya kukubali mwaliko au kufanya mapatano yoyote, anazungumza na mke wake kisha anaamua, huku akifikiria faida zao wawili. Katika hali kama hiyo, usawaziko unasaidia.—Met. 13:10.
Nyakati nyingine watu wanaofunga ndoa wana malezi na tamaduni mbalimbali. Katika hali hiyo, wanahitaji sana kuwasiliana waziwazi. Njia za kuwasiliana zinatofautiana. Kuchunguza jinsi mwenzi wako wa ndoa anavyozungumza na watu wake wa ukoo kunaweza kukusaidia kumfahamu vizuri zaidi. Nyakati nyingine mawazo ya ndani ya mtu hayafunuliwi na jambo analosema bali jinsi anavyolisema. Na yale yasiyosemwa yanaweza kutufunza mambo mengi sana. (Met. 16:24; Kol. 4:6) Utambuzi ni wa maana sana ili kupata furaha.—Soma Methali 24:3.
Kuhusu kuchagua tafrija na burudani, watu wengi wameona umuhimu wa kubadilikana. Kabla ya kufunga ndoa, huenda mwenzi wako alitumia wakati wake katika michezo au burudani fulani. Je, ni muhimu kufanya marekebisho fulani sasa? (1 Tim. 4:8) Swali hilo linahusu pia wakati unaotumiwa pamoja na watu wa ukoo. Inaeleweka kwamba wenzi wa ndoa wanahitaji wakati ili wafanye mambo ya kiroho na shughuli nyingine pamoja.—Mt. 6:33.
Mwanamume anapooa, anaacha baba yake na mama yake, na mwanamke pia anafanya hivyo. (Soma Mwanzo 2:24.) Hata hivyo, mwongozo wa Mungu kuhusu kuwaheshimu baba na mama bado unatumika hata baada ya mtu kufunga ndoa. Hivyo hata baada ya watu kuoana, inaelekea watatumia wakati fulani pamoja na wazazi au wakwe zao. Mume mmoja, ambaye amekaa katika ndoa kwa miaka 25, anasema hivi: “Nyakati nyingine, ni vigumu kusawazisha mapendezi na mahitaji mbalimbali ya mwenzi wa ndoa na yale ya wazazi, ndugu na dada zako, na wakwe zako. Andiko la Mwanzo 2:24 limenisaidia sana kushughulikia hali hiyo. Mtu anapaswa kuwa mshikamanifu na kuwa na wajibu kuelekea washiriki wengine wa familia, hata hivyo, andiko hilo limenionyesha kwamba ninapaswa kwanza kuwa mshikamanifu kwa mwenzi wangu.” Kwa sababu hiyo, wazazi Wakristo wenye usawaziko watatambua kwamba watoto wao waliofunga ndoa wamo katika familia ambamo mume ndiye aliye na wajibu wa kuiongoza.
Kujifunza Biblia kwa ukawaida katika familia ni jambo la maana sana. Mambo yaliyoonwa katika familia nyingi za Kikristo yanathibitisha jambo hilo. Huenda isiwe rahisi kuwa na funzo kama hilo au kulidumisha. Mume fulani anakiri hivi: “Ikiwa tungerudi nyuma na kubadili kila kitu, tungehakikisha kwamba tunajifunza kwa ukawaida kama familia tangu mwanzo wa ndoa yetu.” Anaongeza hivi: “Ni jambo lenye kupendeza kama nini kuona shangwe ambayo mke wangu anaonyesha anapochochewa na kweli fulani zenye kupendeza za Biblia tunazojifunza pamoja katika funzo letu!”
Msaada mwingine ni kusali pamoja. (Rom. 12:12) Mume na mke wanapoungana pamoja katika ibada ya Yehova, uhusiano wao wa karibu pamoja na Mungu unaweza kutia nguvu vifungo vyao vya ndoa. (Yak. 4:8) Mume mmoja Mkristo anasema hivi: “Kuomba msamaha haraka na kutaja makosa mnaposali pamoja ni njia moja ya kuonyesha kwamba mnahuzunikia kikweli hata jambo dogo linaloudhi.”—Efe. 6:18.