Sunday, July 12, 2009

SALA YA MUME AKIMWOMBEA MKEWE

Hapa nimejaribu kubadili maneno kutoka kwenye ila sala ya kumwombea mke au niseme ni kama mfano vipi mume anaweza kumwombea mke wake.


Ee Bwana, wakati mwingine namtazama mke wangu Nami nashangazwa.
Inakuwa kama ni kwa bahati tu nilikutana naye.Siku ile ya kwanza,
Tulikutana na kila mmoja alikuwa mgeni kwa mwenzake.Sasa ninamjua sana.
Lakini bado ninashangaa na kujiuliza.Bila yeye ningekuwa mtu wa namna gani?
Ningefanya nini?

Je? Ningekuwa nimefanya mambo mengi hivyo?
Je? Ningekuwa bado nikitafuta?
Nikitafuta anasa mbaya za maisha, nikiondoa upweke na uchungu,
Kwa chupa moja ya bia baridi au kwa kumtembelea rafiki.

Ninajua kwamba nimebadilika, yeye alinibadilisha.
Upendo wake, na upole wake, kunitunza kwake, na subira yake,
Vimenifundisha na kunijenga.Amenifundisha niwe zaidi,
Niwe zaidi mtu yule uliyetaka niwe.Amenisaidia niwe hivyo
Mlifanya kazi pamoja, ulifanya kazi ndani yake
Naye katika wewe

Ninyi -wawili- Bwana,
Mlinipa moyo, mlinipa nguvu,
Mlinipa amani ya kweli, raha na furaha.
Mlinisaidia, nikajiamini.

Na nikakuamini.
Kwani, Ee Yesu mpendwa, ulikuwa mgeni.
Picha kwenye kitabu, Mtu aliye angani mbali nami.
Mpaka nilipokutana naye.

Kwani alinionyesha nafsi yangu mwenyewe. Na alinionyesha wewe.
Alinipa watoto, watoto wako Ee Bwana. Sasa ni watoto wetu

Hali hii tuliyo nayo leo hii, ni dalili ya upendo wako,
Ninakushukuru kwa ajili yake,umbariki na unlinde.
Umweke salama, na unifundishe jinsi ya kumpenda zaidi.


NAPENDA KUWATAKIENI WOTE JUMAPILI NJEMA

3 comments:

Nicky Mwangoka said...

Asante kwa matashi mema ya Jumapilli. Pia kwa sala nzuri mno kwa mke mwema.Una kipaji Yasinta!
Jpili njema nawe pia

Anonymous said...

sio mchezo

Unknown said...

Ni sala nzuri.....