Friday, July 3, 2009

HII SASA KALI PUNDAMILIA KUKIMBIZA ASKARI (WANAJESHI)


Je? hapa nani kamwingilia nani?

10 comments:

Mwanasosholojia said...

Kweli hii kali, swali moja..pundamilia akiwakamata (hata mmoja wao maana si rahisi kukamata wote..) atafanya nini?atawatafuna au?

Born 2 Suffer said...

Laaah jamaa wanaondoka spidi wanafaa kuchukuliwa katika michezo mbio.

Albert Kissima said...

Da! Kumbe pundamilia ni wanyama wakali hivi?
Halafu dada Yasinta una makusudi wewe, yani badala ya kuwasaidia wanajeshi hao kukabiliana na pundamilia, wewe ukakimbilia kupiga picha.(hahahahahaaaaaa)

Fadhy Mtanga said...

Jamaa hao magwanda waonezi sana ukiingia katika kumi na nane zao. Sasa wao wameingia za watu, lazima watoke nduki.

Mija Shija Sayi said...

Mnyama ni myama tu, sijui walikuwa wanajiamini nini. Wanajeshi ndio watakuwa wachokozi, au unaonaje da'Yasinta?

Yasinta Ngonyani said...

Mwanasosholojia karibu tena kakangu.Ni swali nzuri ila jibu sina kwani sikujua kama Pumbamilia wanafukuza watu.

Born 2 Suffer ni kweli hao wanafaa kuwa kwenye michezo ya mbio.

Kissima, katika kushangaa ninkaona ni bora nipige hii picha kwani sikujua kama ni wanyama wakali.

Ni kweli kaka Fadhi kazi kwelikweli.

Da Mija nakubalia nao kama wasingewachokoza basi asingewakimbiza. Huona hata kuku tu anakimbiza ukimchokoza. Asanteni sana wote kwa kuitembelea blog MAISHA mara kwa mara.Tupo pamoja na Upendo daima.

Bennet said...

Pamoja na kupiga mateke pia wanauwezo wa kung'ata lakini mpaka uwe umembana wewe na sio kukukimbiza kama hivi

mzee wa matukiodaima habari bila uoga said...

Kweli hii ni kiboko binafsi sijapata kuona Pundamilia akifukuza watu kiasi hiki kwa mara ya kwanza nashuhudia kupitia picha hii nzuri hongera

chib said...

Nimeishi katika mbuga ya Ngorongoro kwa miaka 2 nikiwa mfanyakazi katika sekta ya afya, sikuwahi kuona pundamilia wakikimbiza binadamu, nilichoshuhudia ni kuwa wakiona simba huwakimbilia binadamu kwa usalama wao.
Hao askari hawafai kabisa katika jeshi

Anonymous said...

pundamilia alikuwa anafukuzwa na simba (hayupo pichani) ila mwanajeshi naye alimuona ndio maana katoka nduki